Tuesday 19 April 2016

WANAUME TUNAONEWA SANA NA WAKINA MAMA, SEMA TUPO KIMYA, WAO NDO WANAPIGA KELELE KILA SIKU NDO MAANA INAONEKANA WANAONEWA, KAMA UNABISHA HEBU SOMA NAAMINI UTAKUBALIANA NA MIMI

.
1-Wanaume tunatakiwa kufanya kazi kwa bidii ili tuweze kula, kupendwa, kuoa (si unajua mahali inatakiwa), kutunza familia, wakati mwanamke anachotakiwa kufanya ni ku graduate chuo tu ili aweze kuolewa na kupata kila anachotaka.
2-Kwenye familia sisi ndo tunatakiwa kutoa maamuzi magumu yahusuyo familia, mwanamke yeye hukaa pembeni na hii ndo sababu watoto wengi huchukia sana baba zao.
3-inatakiwa tufanye mambo mengi ya kipuuzi ili kuwavutia wanawake (kwa mfano wale wabeba nondo), kupoteza hela zetu tunazopata kwa taabu sana (mfano shopping demu anataka ikafanywe Mlimani City), tunanunua zawadi kuwapelekea kuliko wao wanavyofanya wakijitaidi ni mara moja moja tu na wakati mwingine zawadi zetu wanazikataa au kuzichoma (umkakaeona wapi mwanaume kakataa zawadi ya mwanamke),
kutukejeli, kutucheka ni jambo la kawaida sana kutufanyia( ukibisha wakute wakiwa wanapiga stori)
4-Sisi ndo tunaofanya kazi ngumu, kupigana vita na kuuwawa na bado wanatudharau, HIvi unajua ni mara ngapi nimewapisha wanawake wakae kwenye siti yangu ndani ya daladala? bado waliniona mimi ni mbulula tuu.
5-kwenye familia wanaume ndo tunabeba majukumu yote yahusuyo kutoa pesa (billi ya maji, umeme, ada za watoto shule, shopping..... aiseeee) na wakati mwingine unaweza kukuta mwanaume huna hata pea mbili za viatu za kubadilisha.
6-wanapoamua kutuacha na kuvunja ndoa lazima waende mahakamani kudai hela zetu kwamba tugawane nusu kwa nusu pamoja na mali. na kama hiyo haitoshi wakiamua kuondoka na watoto huwezi pinga mbele ya sheria.
7-tukiwa faragha(kwenye mambo yetu yale) sisi ndo tunabeba jukumukubwa aiseee, wao huwa unakuta wamejilaza tuu (bora wanawake wa pwani wanjituma kidogo), nikiwa bado kwenye hii kitu, sisi ndo wakati mwingine tunalipia hii kitu (wanawake kulipia kwa ajili ya sex bado sijaona, hawapo)
8-Inapotokea ugomvi, moja kwa moja hisia za wengi wanafikiria
wanaume ndo wakorofi ata kabla hawajasikiliza kinacho husika.
9-Hata tukiwa chuoni, mwanaume usitegemee upendeleo wa aina yoyote ile, loh ila kwa wanawake ni kazi ndogo sana... akiachia miguu kwa lecturer unadhani kuna Disco apo?
Kwa kifupi wanawake wanachotakiwa ni kuwa na muonekano mzuri tu.Lakini mwanaume ukiwa ata na muonekano mzuri bila kutoka jasho na kujituma lazima uitwe SHOGA.
Hivi jamani nani. anaonewa apo?

No comments:

Post a Comment