Saturday 23 April 2016

DAR ES SALAAM SCHOOL OF JOURNALISM (DSJ)


LEO ASUBUHI WANAFUNZI WA CHUO CHA UANDISHI WA HABARI (DSJ) NGAZI YA STASHAHADA- A MWAKA WA KWANZA
WALIKUWA NA ZIARA MAALUMU "DSJ -PR ASSOCIATION 2016"
KWAAJILI YA KWENDA SHULE YA MSINGI UHURU MCHANGANYIKO KWAAJILI KUTEMBELEA WATOTO WALIOWALEMAVU NA KUSAIDIA KUTOA MICHANGO MBALIMBALI YA MAHITAJI

MICHANGO ILIYOTOLEWA NA DSJ:

SUKARI, SABUNI YA UNGA,SABUNI YA KUOGEA, DAWA YA MSWAKI, PENCILS, MAFUTA YA KUPIKIA, MAFUTA YA KUPAKA, JUICE , CHUMVI, N.K

PAMOJA NA "PED" KWA UPANDE WA  WANAFUNZI JINSIA YA KIKE WALIOFIKIA UMRI WA KUELEKEA UTU UZIMA

PIA DSJ ILITOA MCHANGO WA PESA KWAAJILI YA KUTENGENEZEA MASHINE TANO (5) ZA KUSOMEA WANAFUNZI WASIOWEZA KUONA

MRATIBU WA MASOMO CHUO CHA DSJ MADAM JOYCE MBOGO
AMEWAPONGEZA UONGOZI WA SHULE YA MSINGI 'UHURU MCHANGANYIKO'
KWA KUKUBARI KUWA PAMOJA NA CHUO CHA DSJ KWA SIKU YA LEO KATIKA SHIRIKIANA KUSAIDIANA NA KUWATEMBELEA WATOTO (WANAFUNZI WALIOWALEMAVU)
AMETOA SHUKRANI ZA DHATI KWA MWALIMU MKUU WA SHULE YA UHURU MCHANGANYIKO

IMETOLEWA NA CHUO CHA UANDISHI WA HABARI (DSJ)

Thursday 21 April 2016

Kazi na Sikukuu

Likizo yenye malipo

Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya 2004 inatoa livu ya kila mwaka baada ya kukamilisha mwaka mmoja wa huduma na mwajiri. Mfanyakazi anastahili siku 28 za livu yenye malipo ya kila mwaka, pamoja na sikukuu zozote za kitaifa ambazo zinaweza kuwa wakati wa kipindi hicho cha livu. Livu ya kila mwaka inaweza kupunguzwa na idadi ya siku wakati wa mzunguko wa livu, ambazo hutolewa kama livu yenye malipo na mwajiri iwapo mfanyakazi atakubali.
Mfanyakazi mwenye miezi chini ya sita kazini hatakuwa na haki ya kupata likizo yenye malipo chini ya masharti ya ajira na mahusiano kazini. Hii haita husisha mfanyakazi aliyeajiriwa kwa msingi wa musimu au mfanyakazi, mwenye utumishi wa chini ya miezi sita na ambaye amefanya kwa zaidi ya mara moja katika mwaka.
Mwajiri anaweza kuamua muda wa livu ya kila mwaka bora livu hiyo isizidishe miezi sita baada ya muda wake kufikia. Muda wake unaweza kuongezwa hadi kipindi cha miezi 12 iwapo mfanyakazi atakubali na ikiwa kirefusho hicho kinakubaliwa na mahitaji ya utendakazi ya mfanyakazi.
Huenda mwajiri asimruhusu mfanyakazi kuchukua livu ya kila mwaka kwa niabaya livu nyingine ambayo mfanyakazi anastahili. Huenda mwajiri hasihitaji au kuruhusu mfanyakazi kufanya kazi wakati wa livu ya kila mwaka. Mfanyakazi anastahiki mishahara yake ya kawaida wakati wa kipindi chake cha livu ya kila mwaka. Lazima malipo yalipwe kabla ya livu kuchukuliwa.
Mwajiri amekatazwa kulipa fidia inayotokana na livu ya kila mwaka isipokuwa wakati wa kukatishwa kwa ajira au kuisha wa kila kipindi kulingana na mfanyakazi aliyeajiriwa kulingana na msimu. Kando na toleo hili, makubaliano yoyote yanayotoa fidia kwa niaba ya livu ya kila mwaka ni batili na sio halali. Kiwango cha fidia uhesabiwa kwa kiwango cha mshahara wa kawaida wa siku kwa kila siku 13 ambazo mfanya kazi alifanya kazi au alistahili kufanya kazi.
Chanzo: Sehemu ya 29-31 ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya 2004.

Malipo siku za mapumziko kitaifa

Wafanyakazi wana haki ya kuendelea kulipwa ujira wao  wakati wa mapumziko ya kitaifa (za dini na za kiserikali). Siku za mapumziko kwa kawaida hutangazwa na serikali (kwa kawaida zipo siku za mapumziko 17 kwa mwaka).
Siku za mapumziko husimamiwa na sheria ya Siku za mapumziko ya mwaka wa 1966. Hujumuisha siku zifuatazo za mapumziko ya kitaifa. Mwaka mpya (1 Januari), Siku ya Mapinduzi ya Zanzibar (12 Januari), Siku ya Maulidi (Januari 03), Ijumaa kuu (Aprili 03), Jumapili ya Pasaka (Aprili 05), Jumatatu ya Pasaka (Aprili 06), Siku ya Sheikh Abeid Amani Karume ( Aprili 07), Siku ya Muungano (Aprili 26), Siku ya wafanyakazi (Mei 01), Siku ya Maonyesho ya Kibiashara ya Kimataifa/ Saba Saba (Julai 07), Nane nane (Wakulima) (Agosti 08), Eid-el-Fitri( Julai 17 ), Siku ya Mwalimu Nyerere (Oktoba 14), Idd-El-Hajj (September 23), Siku ya Uhuru na wa Jamhuri ya Tanzania (Desemba 09), Siku ya Krismasi (Desemba 25), Boxing Day (Desemba 26). Sikukuu za kiislamu zinategemea sana mwandamo wa mwezi na kwa hivyo zinaweza kubadilika.
Sikukuu zinazokuwa Jumamosi au Jumapili huzingatiwa siku hizo. Sheria Nambari 10 ya 1994 ime badilishwa na sikukuu zinazokuwa Jumamosi au Jumapili hazifidiwi tena.
Chanzo. Sheria ya Siku za Mapumziko ya mwaka wa 1966

Siku ya Mapumziko ya juma

Wafanyakazi wana haki ya kupata saa 24 mtawalia za mapumziko kila wiki kati ya siku ya mwisho ya kufanya kazi katika wiki moja na siku ya kwanza ya kawaida ya kufanya kazi ya wiki inayofuata. Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini inahitaji kwamba siku ya mapumziko ya kila wiki, kikanuni, inapaswa kuwa Jumapili kwa wafanyakazi wote.
Makubaliano yaliyoandikwa yanaweza kutoa kipindi cha mapumziko cha angalau saa 60 mtawalia baada ya wiki mbili au kipindi cha mapumziko cha kila wiki kinaweza kupunguzwa hadi saa 8 ikiwa kipindi cha mapumziko katika wiki inayofuatia kimeongezwa kwa usawa.
Chanzo: Sehemu ya 24 ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya 2004.

Taratibu juu ya Kazi na Sikukuu

  • Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Sehemu ya 6 ya 2004 / Employment and Labour Relations Act, No. 6 of 2004
  • Sheria ya sikukuu za kitaifa, 1966 / Public Holidays Ordinance, 1966

Fidia


Malipo kwa masaa ya ziada ya kazi

Kwa mujibu wa Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka wa 2004; mfanyakazi anaweza akahitajika kufanya kazi kwa siku 6 kwa juma. Masaa ya kazi ya kawaida kwa siku na juma ni saa 9  kwa siku na saa 45 kwa wiki isipokuwa kwa wale ambao wanawasimamia wafanyakazi wengine kwa niaba ya mwajiri na ambao wanaripoti moja kwa moja kwa usimamizi mkuu. Huenda wafanyakazi wakahitajika kufanya kazi kwa saa za ziada, kufanya kazi zaidi ya saa za kawaida za kufanya kazi, lakini sio zaidi ya saa 12 kwa siku na saa 50 katika mzunguko wa wiki 4 isipokuwa katika hali ya dharura. Mkataba ulioandikwa utatakiwa kumtaka au kumruhusu mfanyakazi kufanya kazi mpaka saa 12 kwa siku, ikijumuisha kipindi cha kula, bila kupokea malipo ya masaa ya ziada. Makubaliano hayo hayatakiwi kumtaka au kumruhusu mfanyakazi kufanya kazi- (a) kwa zaidi ya siku tano kwa wiki; (b) kwa zaidi ya saa 45 kwa wiki; (c) kwa zaidi ya saa ya ziada 10 kwa wiki.
Mkataba wa pamojo unatakiwa kutoa wastani wa saa za kawaida na saa za ziada za kazi kwa kipindi kilichokubaliwa (kisichozidi mwakaa mmoja) hata hivyo mkataba kama huo hautakiwi kumtaka au kumruhusu mfanyakazi kufanya kazi kwa zaidi ya wastani wa saa 40 za kawaida kwa wiki zikihesabiwa kwa kipindi kilichokubaliwa na saa kumi za ziada kwa wiki zikihesabiwa kw kipindi hicho kilichokubaliwa.
Kikomo cha saa za ziada hakitumiki kwa wafanyakazi wanaowasimamia wafanyakazi wenzao kwa niaba ya mwajiri na ambao wanaripoti moja kwa moja kwa usimamizi wa juu; au kazi ya dharura ambayo haiwezi kufanywa na wafanyakazi wakati wa saa za kawaida za kazi; na au pale ambapo makubaliano ya pamoja yanatoa mwongozo wa kuwa na wastani wa saa za ziada za kazi kwa kipindi kilicho kubaliwa kisichozidi mwaka mmoja, kulinga na kikomo cha wastani cha saa 10 za ziada za kazi kwa wiki.
Ikiwa mfanyakazi anafanya kazi zaidi ya saa zilizowekwa za kufanya kazi, anastahiki malipo ya saa za ziada ambfazo ni saa moja na nusu (1.5 ya X au 150%) ya kiwango cha malipo yake ya kawaida.
Chanzo: Sehemu ya 17-22 ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya 2004

Fidia kwa kazi za Usiku

Kulingana na Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, usiku ni kipindi kati ya 20.00 na 06:00 (ya siku inayofuatia).
Kazi ya usiku hulipwa kwa kiwango cha asilimia 5% juu ya kiwango cha kawaida cha mshahara. Ikiwa kazi ya usiku imefanywa kama kazi ya ziada, saa hizo za ziada hulipwa kwa kiwango cha usiku (ambacho ni asilimia 105% cha kiwango cha kawaida cha siku).
Chanzo: Sehemu ya 20 (4) ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya 2004

Mapumziko ya Fidia kwa kufanya kazi siku za mapumziko

Sheria haitamki wazi ikimtaka mwajiri kutoa mapumziko ya fidia kwa mfanyakazi aliyefanya kazi siku ya mapumziko ya Juma au Kitaifa. 

Fidia ya kufanya kazi siku za mapumziko ya Juma au Sikuu za Kitaifa

Huenda wafanyakazi wakahitajika kufanya kazi katika siku za kupumzika za wiki na siku za mapumziko. Katika hali kama hizo wakati wafanyakazi wanalazimika kufanya kazi siku rasmi za mapumziko, wanastahiki kupokea mishahara kwa kiwango cha asilimia 200% cha kiwango cha kawaida cha mshahara wa kila saa. Wafanyakazi wanaofanya kazi katika siku za kupumzika za kila wiki wanastahili malipo kwa kiwango cha asimila 200% cha kiwango cha kawaida cha mshahara.
Chanzo: Sehemu ya 24 na 25 ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya 2004, Sehemu ya 7 ya Agizo la Mishahara 2010

Taratibu juu ya fidia

  • Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Sehemu ya 6 ya 2004 / Employment and Labour Relations Act, No. 6 of 2004

Fahamu haki na wajibu wa mfanyakazi kisheria

Huwezi kudai kitu ambacho hufahamu kuwa kipo na hata kama unajua kipo hujui kinapatikanaje na hata kama unajua kinavyopatikana hujui nani anawajibika kukupatia.
Kama kuna jambo la muhimu kwa mfanyakazi, kabla ya kazi yenyewe na mshahara atakaolipwa ni kujua haki zake na wajibu wake kisheria.
Kwa mujibu wa Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya Mwaka 2004, kanuni za ajira na uhusiano kazini za Mwaka 2007 pamoja na Sheria ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi ya Mwaka 2003 na marekebisho yake; mfanyakazi anazo haki nyingi ambazo anapaswa kuzifahamu na kuzipata.
Haki hizi ni pamoja na kupatiwa mkataba wa kazi, kufahamu ameajiriwa katika nafasi gani na majukumu yake yatakuwa ni yapi, ili asije akafanya majukumu yasiyomhusu. Mfanyakazi ana haki ya kwenda likizo (siku 28) ndani ya kila mzunguko wa miezi 12, kupatiwa likizo ya matibabu (siku 126) endapo ataugua. Likizo ya uzazi ambayo kwa mwanamke ni siku 84 kwa mtoto 1 na siku 100 kwa mtoto zaidi ya 1. Mwanamume likizo ya uzazi ni siku 3.
Mfanyakazi ana haki ya kulipwa malipo stahiki yanayoendana na kazi anayofanya na kiwango kilichowekwa na Serikali kwa mujibu wa sheria. Hii ni pamoja na malipo ya muda wa ziada.
Endapo mfanyakazi ataumia akiwa kazini ana haki ya kuhudumiwa kwa matibabu na mwajiri pamoja na kulipwa fidia ya madhara aliyoyapata. Mfanyakazi ana haki ya kupatiwa vitendea kazi na mazingira rafiki ya kufanyia kazi siyo hatarishi. Kutobaguliwa, kutonyanyaswa, kutonyanyapaliwa, kutotengwa, kutodhalilishwa kijinsia na kutopigwa ni mojawapo ya haki za mfanyakazi. Mfanyakazi yuko huru kujiunga na chama cha wafanyakazi.
Mfanyakazi ana haki ya kuvunja mkataba wa kazi kwa kufuata utaratibu uliowekwa kisheria. Endapo mfanyakazi ataachishwa kazi au kustaafishwa, anaweza kuwa na haki ya kulipwa malipo ya notisi, kiinua mgongo, usafiri, cheti cha utumishi, mafao ya hifadhi ya jamii, malimbikizo ya likizo na malipo mengineyo. Mfanyakazi pia ana haki ya kugoma baada ya kufuata utaratibu wa kisheria, ili kushinikiza madai yake kutekelezwa au ili kufikisha ujumbe kwa mwajiri.
Sheria pia imeweka wazi wajibu wa mfanyakazi kuwa ni pamoja na kufanya kazi kwa bidii, kufikia malengo ya mwajiri, usiri, utii, nidhamu na uaminifu. Kutoa taarifa kwa maandishi mapema tatizo linapotokea wakati wa ugonjwa, ajali au kuibiwa.
Kutoa notisi au malipo unapotaka kuacha kazi, kutoa taarifa ya kujifungua kabla ya mwezi husika, kuwa mbunifu na kulinda masilahi ya mwajiri wakati wote, kufuata utaratibu za kisheria wakati wa migomo na kutumia njia za kidiplomasia kutatua migogoro na mwajiri badala ya njia za uvunjifu wa amani. Kumbuka kila haki inaambatana na wajibu. Kabla hujadai haki zako timiza kwanza wajibu wako. Pia, wakati mwingine haki haipatikani kirahisi, kwa nidhamu ya woga au kwa maneno pekee. Kuwa jasiri, jenga hoja, dai haki zako kwa kufuata utaratibu na sheria ya kazi.
-

Wednesday 20 April 2016

Kama Unatafuta Kazi,..Haya Ndiyo Mambo Muhimu Ya Kukusaidia Kupata Kazi hiyo.


Wengi wetu mara tunapomaliza masomo huwa tunatafuta ajira kwa njia mbalimbali. Kuna wakati tunaandika barua za maombi na kusubiri, kuna wakati tunasaidiwa na jamaa zetu kupata ajira na kuna wakati tunapita ofisi moja hadi nyingine kuomba ajira.
Katika kutafuta ajira, kama ilivyo katika shughuli nyingine, kuna kanuni. Hebu  tuchukulie wewe ni  kijana na ndiyo kwanza umemaliza masomo yako ya chuo na umeenda kwenye usaili (Interview) kwa ajiri ya kupata ajira. Unafikiri hasa ni mambo gani ambayo unatakiwa kufanya?
Hebu tuanze na kujiamini. Hakuna kitu utakachosema wakati wa usaili kinachoweza kuwa na umuhimu kama mwenyewe hutaonekana mtu mwenye kuaminika. Kiongozi wako mpya wa kazi ni lazima akuamini. Hakuna mtu aliyetayari kuajiri mtu ambaye anajua hatomwamini. Sasa ni vipi utajenga kuaminika?
Kwanza ni muhimu uzungumze ukweli. Wapo watu wenye uwezo wa kuongopa vizuri sana na wasigundulike. Lakini hawa ni wachache sana. Wengi wetu huweza kujikuta tukigundulika kwamba hatusemi ukweli.
Unajua jinsi ambavyo hata wewe mwenyewe umewahi kuzungumza na mtu na kuhisi kwamba anachokueleza si ukweli. Hilo ni tatizo la wengi wetu na wala usidhani ni tatizo la huyu mtu aliyekuwa akikueleza wewe tu.
Kama unajiamini na unaamini ukweli wa kile unachosema. Hata uwe mtu mwenye tabia ya wasiwasi kiasi gani, hali ya uwazi na usahihi wa mazungumzo yako itaonekana wazi.
Pili, unatakiwa kuwatazama machoni unaozungumza nao. Huna haja ya kuishangaa miguu yao, ama kushangaa kikombe kilichowekewa kalamu juu ya meza ya msaili wako au kushangaa feni iliyo kwenye dari la chumba cha usaili
Fanya kila jitihada umtazame moja kwa moja msaili au wasaili na uzungumze katika hali ya kawaida iwezekanavyo. Hakutakuwa na  tatizo kuwatazama machoni wakati unapeana mikono na kuwaeleza, ‘samahani, kidogo mimi mimi nina tatizo la kukumbwa na wasiwasi kirahisi’. Kama ni msaili au wasaili ni wenye busara, ni lazima watazungumza kitu chenye lengo la kukutoa wasiwasi.
Lakini ikiwa msaili ataonesha kukudharau kwa kauli yako hiyo ya ukweli, basi kuwa na uhakika kwamba hata ukipata nafasi unayotaka hutofurahia kufanya naye kazi.
Unataka kumvutia mkuu wako mtarajiwa wa kazi pamoja na wafanyakazi wenzako, kama vile wewe unavyopenda majukumu yako. Hivyo, kuwa wazi na mwaminifu katika kipindi chote cha usaili, na kumbuka kwamba unayo nafasi ya kuwasaili wao pia kama wakuu wako wa baadaye wa kazi, na wala si jambo la upande mmoja. Kama ilivyo kwako, nawe unatakiwa kuwa na hakika kama utafanya nao kazi vizuri.
Hebu sasa tutazame picha kwa ujumla ya namna unavyoweza kujtafutia soko na kujitambulisha kama mtu mwenye uwezo wa kazi, mwenye uwezo wa kutegemewa, mwenye akili, mwaminifu na rasilimali nzuri za baadaye  kwa kampuni.
Kwanza, huwezi kuanza kuomba kazi, bila kujiamini kwamba una vitu vyote hivyo. Mkesha wa siku ya usaili, pitia mambo yote muhimu ambayo mkuu wako wa kazi angepennda uwe nayo kama mfanya kazi wake.
Chukua nafasi ya mkuu wako huyo wa kazi akilini mwako na ufikirie kama ungekuwa wewe ni vitu gani ungetafuta kama mfanyakazi wako mpya. Unaweza kufanya majaribio ya usaili na ukiweza, mpate rafiki yako atakayekusaidia kufanya hivyo.
Unaweza kujiuliza maswali yafuatayo…Nina uwezo? Ninao utaalamu wa msingi unaotakiwa ili kuweza kuifanya kazi hii ama nahitaji mafunzo zaidi? Ni vipi nitaweza kujifunza kwa haraka.
Haitakuwa vibaya sana kwako kama ukienda zaidi ya uwezo wako wa sasa na kujaribu kutazama mambo yanayoweza kuwa changamoto. Lakini unatakiwa kuwa mwaminifu na huna haja ya kujidai tayari unaweza kila kitu, kwa kiwango cha juu kabisa, wakati una hakika si hivyo.
Endelea na orodha ya maswali…Je wewe ni mtu wa kutumainiwa? Ni uwezo upi mpya mbali na yale uliyoorodhesha kwenye orodha ya mahitaji ya kazi utakaouleta kwenye kampuni? Uwe tayari kumweleza msaili wako mambo ya ziada ambayo kampuni itafaidika nayo ikiwa itakuajiri.
Rudia majibu yajo kwa msaili wako wa kufikirika, ili utakapoingia kwenye chumba cha usaili uwe tayari na mawazo ya kile utakachomweleza msaili wako ili kujitafutia soko vizuri.
Kwa kuwa na majibu yako yaliyotayarishwa, utakuwa na wakati rahisi wa kujitambulisha kama mtu mwenye busara na akili hata kama una kawaida ya kuogopa sana pale usaili wa kweli unapoanza.

SOMA; Dalili 8 Za Kutofanikiwa Kwa Kile Unachofanya.

Mwisho, usijaribu hata siku moja kuonyesha kutokujiamini. Wahi muda uliopangwa, vaa nguo zinazohitajika kwa ajili ya kazi uliyoomba, jua jina la kampuni unayoomba kazi, kazi unayoomba, na mfahamu anayekusaili.
Ni vema ukawahi na kujua zilipo huduma nyingine za muhimu kama choo, bafu na kadhalika. Huna haja ya kulijaza tumbo lako na vitu vya majimaj ama chakula.
Baadhi ya mambo haya yaweza kuonekana ya kijinga, lakini hakuna kitu kibaya kama kuonekana ukihangaika kwenye kiti ulichoketi kutokana na usumbufu wa tumbo ama kibofu chako cha mkojo, wakati unatakiwa kuonekana mwenye kujiamini, uliyetulia na uliyetayari kwa usaili.
Kuwa macho na namna unavyozungumza. Epuka kutumia maneno makali na lugha ya mtaani. Kuwa macho na lafudhi. Usiruhusu lafudhi ya ajabu au sauti iliyosikia ikufanye ukose kazi uliyokuwa ukiitoa siku zote.
Kumtumia rafiki yako kwa usaili wa majaribio, kwa weza kukusaidia kuongeza sana kujiamini wakati msaili wako wa kweli atakapokuwa mbele yako. Kama kweli unajiamini, kujitafutia soko hakuwezi kuwa jambo gumu. Fanya mazoezi kwa kile unachotaka kukisema.
Kama kweli hujiamini, basi ni bora ukafanya jitihada za kuondoa tatizo hilo kwanza. Kama lengo ni kujijengea maisha mazuri na ya furaha, basi iko haja ya wewe nawe kuwasaili wanaotaka kukuajiri ili kujua kama watafaa kukujengea maisha hayo ya furaha baadaye. Unatafuta mwajiri aliyetulia na rahisi kufanya naye kazi.
Kwa makala nyingine nzuri hakikisha unatembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza zaidi kila siku.
Tunakutakia kila la kheri katika mafanikio ya kazi unayoitafuta.
Ni wako rafiki katika mafanikio,

Sababu Zinazofanya Watu Wengine Kuwa Waongeaji Sana Bila Kuwa Watekelezaji Wa Mipango Yao.


Ni mara nyingi katika maisha yako umewahi kusikia au kuona watu ambao ni waongeaji sana wazuri wa mipango na malengo yao. Watu hawa wanapokuwa wanaongelea mipango, mikakati na malengo yao kwa hakika ni mipango mizuri ambayo ikiwekwa kwenye vitendo ni lazima kufanikiwa kuwepo.
Lakini pamoja na kuwa na mipango hiyo mizuri ambayo huwa ina uwezo wa kuwatoa watu hao hata kwenye umaskini unaowazunguka kwa bahati mbaya sana watu hao huwa siyo watekelezaji wa mipango hiyo mizuri  hujikuta ni watu kuongea tu bila kufanya kitu chochote. Hawa ni watu ambao tunao karibu kila siku na tunawajua.
Sasa kitu cha kujiuliza kwa nini watu hawa, mara nyingi huwa ni waongeaji tu bila kutekeleza kitu chochote. Kwa kawaida huwa yapo mambo yanasababisha kwa namna moja au nyingine na kujikuta wakiwa ni watu ambao hawafanyi kitu katika maisha yao. Sababu hizo huwa ni kama zifuatazo:-
1. Kutaka kujionyesha.
Wengi wa watu hawa kwa kutaka kwao sifa, na kujiona wako juu kimaisha mwisho hujikuta  ni watu wa kuongelea sana mipango yao bila kuitekeleza. Hiyo yote huja ili wao kutaka kuonekana kuwa ni watu wa hadhi fulani kumbe sivyo ndivyo. Kwa kadri utakavyojikuta unataka kujionyesha, elewa ndivyo ambavyo utendaji wako utapungua.
Kama unataka kufanikiwa, acha tabia hii mara moja. Maisha yako yanatataka yaonekane katika uhalisia wake na sio kupanga tu bila utekelezaji. Kwa kujifunza na kulijua hili unatakiwa kubadili mwelekeo mara moja na sifa zote kuweka pembeni.
2. Kutokutaka kuwajibika.
Ni kweli hiki ni kitu ambacho kinawafanya watu hawa wawe  ni watu wa kuongea kutokana na wao kutokutaka kuwajibika. Kutokana na hili la ktokupenda kuwajibika ama kujituma hujikuta ni watu ambao wanahamishia nguvu zao nyingi kwenye kuongea badala ya kutenda. Jaribu kuwachunguza wengi utawagundua wako hivi.
Hawa huwa ni watu wanaopenda sana kuonekan ni wasomi na wanajua kila kitu. Kwa sababu ya hiyo wanakuwa ni watu ambao hawawezi kuwajibika ipasavyo na hujikita kwa kushindwa kwao kuwajibika wanakuwa ni watu wa kushindwa kufanya mambo yatakayoweza kuwaletea mabadliko katika maisha yao.

3. Wanasahau mawazo yao mapema.
Pamoja na kuwa watu hawa huwa ni mafundi sana wa kuongea juu ya ndoto zao lakini huwa ni watu wa kusashau sana kile walichokiongea. Na hii huwa inatokea kutokana na wao kutoweza kuyaandika mawazo yao muhimu. Kwa kutokuyaandika mawazo muhimu ambayo wanatakiwa kuyatekeleza ndivyo hujikuta kubaki kuwa waongeaji.
Ili uweze kusonga mbele na kubadili maisha yako ikiwa unajua wewe ni mwongeaji unalazimika sana kuandika mawazo yako muhimu. Kitendo cha kuweza kuandika mawazo muhimu kutakusaidia kukupa hamasa ya kuweza kuzidi kuendelea tofauti na unavyo ongeongea tu, mwisho wa siku utajikuta unabaki kuwa mtu wa kuongea tu.
4. Kukosa hamasa kubwa ya kusonga mbele.
Mara nyingi watu hawa pamoja na kuongea sana lakini huwa ni watu ambao wanakosa hamasa ya kusonga mbele. Kwa nini kitu hiki huwa kinatokea? Hii huwa ni kwa sababu wanakuwa ni waongeaji wao sana kiasi cha kwamba wanajikuta kushindwa kupata ule muda wa kujifunza kwa wengine mambo ya kimafanikio ambayo yanaweza kuwapa hamasa zaidi, huku wakiamini wao wanaweza.
Kutokana na kushindwa kupata muda wa kujifunza kutoka kwa wengine hamasa ya kutenda au kiutendaji kwao hupungua kidogo kidogo na mwisho wa siku hupotea kabisa. Ili kuweza watu hawa kusonga mbele na kuwa watendaji ni lazima wajifunze vitu vipya kwa wengine.
Elewa kuwa, kama utazidi kuwa mwongeaji katika mambo yako sana kuliko utendaji ndivyo unavyofanya maisha yako kuwa magumu na kuyarudisha nyuma. Ni vizuri kulielewa hilo, vinginevyo itakuwa ni ngumu sana kwako kuweza kufanikiwa katika maisha yako.
Kwa makala nyingine nzuri hakikisha unatembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza zaidi.

Tunakutakia kila la kheri katika safari yako ya mafanikio iwe ya ushindi na endelea kutembelea Official Michael Charles Journalist kwa kujifunza na kuhamasika kila siku, karibu.
 

Mambo 6 Yatakayokufanya Uzidi Kuwa Bora Na Mwenye Mafanikio Makubwa.


Habari rafiki na mpenzi msomaji wetu , 
naamini umzima afya na unaendelea na harakati za kuboresha maisha yako. Karibu tena katika siku nyingine ya kujifunza na kuboresha maisha yetu kama ilivyo kawaida yetu. Hili ni jukumu ambalo unatakiwa kuliendeleza karibu kila siku katika maisha yako.
Kumbuka, kama ambavyo tumekuwa tukisema mara kwa mara kupitia mtandao huu wa Official Michael Charles Jornalist  ni muhimu na ni lazima kuwa bora zaidi ili kujihakikishia mafanikio ya kudumu. Kwa wale wasomaji wazuri waOfficial Michael Charles Jornalist wanalijua hili vizuri na umuhimu wa falsa ya kuwa bora kila siku katika maisha yetu.
Na katika kuhakikisha hili linafanikiwa huwa yapo mambo ambayo tunatakiwa tujifunze na kuyafanyia kazi kila siku. Mambo hayo, ambayo unatakiwa uyaelewe na kuyafanyia kazi ili uwe bora siku zote, baadhi tunakwenda kujifunza kupitia makala hii. Je, ni mambo gani yatakayokufanya uzidi kuwa bora na mafanikio makubwa?
Yafutayo Ni  Mambo 6 Yatakayokufanya Uzidi Kuwa Bora Na Mwenye Mafanikio Makubwa.
1. Jielewe mwenyewe.
Hatua mojawapo kubwa itakufanya uzidi kuwaa bora siki hadi siku ni wewe kujitambua kwanza. Kwa kujijua wewe itakusaidia kujua udhaifu wako na kuboresha yale maeneo ambayo kwako unaona yana shida au yana kukwamisha kwa kiasi fulani. Watu wengi huwa wanakwama au kuchelewa kufanikiwa kwa sababu ya kushindwa kujitambua wao mapema na yale mambo yanayo wakwamisha kufikia mafanikio hayo.

USHINDI NI LAZIMA UKIWA BORA SIKU ZOTE
2.  Kuwa na mawazo chanya.
Maisha yako yatakuwa bora zaidi na ya wepesi kama utakuwa mtu wa mawazo chanya. Kinyume cha hapo utageuza maisha yako kuwa mzigo mkubwa ambao utashindwa kuubeba. Hii ndiyo siri mojawapo pia ya kukufanya uzidi kuwa bora kwa kile unachokifanya. Hivyo, chochote unachokifanya kitazame kwa mtazamo chanya, hiyo itakusaidia kuwa bora sana.
3. Kuwa wewe kama wewe.
Utazidi kujihakikishia ubora mkubwa katika maisha yako ikiwa utabaki  kuwa wewe kama wewe. Hakuna mafanikio makubwa yanayoweza kupatikana kwa kuiga. Kumbuka umeumbwa ukiwa wewe kama wewe, hivyo kwa kila unalolifanya acha kuiga sana. Jifunze kuwa wewe kama wewe, kwani kuiga kuna mipaka yake. Ukifanikiwa kumudu hili itakusaidia sana kuwa bora kwenye maisha yako kuliko unavyofikiri.
4. Jiamini.
Siri kubwa ya mafanikio ipo kwenye kujiamini. Mipango na malengo mengi yanashindwa kufanikiwa kwa sababu ya kutokujiamini. Kwa kadri utakavyoweza kujenga nguvu kubwa ya kujiamini itakusaidia sana kuwa bora wakati wote na kuweza kufikia mafanikio makubwa ambayo unayahitaji katika maisha yako. Kwa kujiamini tu, itakusaidia kufikia mafanikio makubwa na kuwa bora zaidi kwenye maisha yako.
5. Kujifunza.
Hitaji la kwanza ambalo litafanya maisha yako yazidi kuwa bora ni kujisomea kila siku. Unatakiwa kujifunza kupitia vitabu, semina au mitandao ya kuhamsisha kama iliyo chini ya Official Michael Charles Jornalist . Kwa bahati mbaya sana tatizo kubwa walilonalo watanzania wengi ni kule kushindwa kujisomea. Wengi hawapo tayari kupata maarifa haya. Kama wewe ni mtu wa kujisomea elewa utakuwa umeachana na kundi kubwa na kufuata njia ambayo itakupeleka kwenye  ubora siku hadi siku.
6. Kuwa msikilizaji mzuri.
Siku zote acha kuzungumza tu, kama unataka kuwa bora jifunze kuwa msikilizaji mzuri pia. Unapokuwa msikilizaji inakusaidia kujua mambo mengi ambayo hapo mwanzo hukuyajua kabisa. kumbuka hata watu wenye mafaniko ni wasikilizaji pia wazuri.
Yapo mambo mengi ambayo yanaweza kukufanya ukawa bora zaidi. Chukua hatua kwa kwa kuyafanyaia kazi hayo ili kufikia mafanikio  yako makubwa.
Endelea kutembelea Official Michael Charles Jornalist

Hatua Tano Za Uhakika Za Kutatua Tatizo Lolote Ulilonalo.


Habari rafiki?
Changamoto ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku, hakuna jinsi ambavyo tunaweza kuondokana na changamoto zote kwenye maisha yetu. Kila siku tutakutana na changamoto ambazo pia zitatuingiza kwenye matatizo mbalimbali.
Watu wengi wanapojikuta kwenye matatizo huchukua hatua ambazo zinazidisha tatizo walilonalo, au kukata tamaa na kuachana na tatizo hilo, kitu ambacho kinafanya tatizo lizidi kuwa kubwa.
Na pia watu wengi ambao wamekuwa wakiomba ushauri juu ya changamoto au matatizo wanayopitia, mara nyingi majibu tayari wanakuwa nayo wao wenyewe. Wanachokwenda kupata kwa washauri siyo majibu mapya, bali wanakwenda kuwezeshwa kutumia majibu ambayo tayari wao wenyewe wanayo.
Unaonaje kama na wewe ungeweza kupata nguvu hiyo ya kuweza kutumia majibu yaliyopo ndani yako kutatua changamoto na matatizo yako? Itakuwa bora sana, na hiki ndicho tunakwenda kujadili kwenye makala hii ya leo.
Kuna hatua tano ambazo kama utazifuata, utapata suluhisho bora la tatizo lolote unalopitia kwa sasa au utakalokuja kupitia kwenye maisha yako. kwa kuzijua hatua hizi itakuwa rahisi kwao kuchukua hatua stahiki kwa jambo lolote unalopitia kwenye maisha yako.
Kabla hatujaingia kwenye hatua hizi tano, kuna kitu kimoja muhimu sana unachohitaji kuwa nacho, na kitu hiki ni kijitabu cha kuandika mambo yako muhimu.
 
Hatua tano za uhakika za kutatua tatizo lolote unalokutana nalo.
Hatua ya kwanza; jua kwa undani tatizo ni nini.
Najua utashangaa lakini ukweli ni kwamba wengi ambao wanakuwa na matatizo huwa hawajui tatizo hasa walilonalo ni nini. Na hivyo wanapokazana kulitatua wanashindwa, kwa sababu kama hujajua kiini cha tatizo huwezi kulitatua.
Mara nyingi watu wamekuwa wakiangalia madhara ya tatizo, badala ya kuangalia chanzo kikuu cha tatizo. Huwezi kutibu tatizo kwa kutibu madhara, badala yake unahitaji kuzama ndani na kujua chanzo hasa cha tatizo ni nini.
Na njia ya uhakika ya kufikia hilo ni kuuliza swali moja muhimu sana, KWA NINI. Uliza swali hili mara tano, yaani uliza kwa hatua tano. Kwa mfano kama tatizo lako ni kipato kidogo kwenye biashara yako, jiulize kwa nini kipato ni kidogo, jibu linaweza kuwa wateja ni wachache, jiulize tena kwa nini wateja ni wachache, hapo utapata majibu mengine, kwa kila jibu jiulize tena kwa nini? Mpaka utafika mahali na kuona hiki ndio kiini kikuu cha tatizo.
Lijue tatizo vizuri, wahenga walisema kulijua tatizo ni nusu ya kulitatua.
SOMA; USHAURI; Hatua Za Kuchukua Pale Unapogundua Umeoa Au Kuolewa Na Mtu Ambaye Tabia Zake Na Zako Haziendani.
Hatua ya pili; orodhesha hatua unazoweza kuchukua.
Baada ya kujua nini hasa ndiyo tatizo, sasa anza kuorodhesha kila hatua unayoweza kuchukua. Andika kila suluhisho linalowezekana kwenye tatizo ulilonalo. Usijihukumu kwamba hiki kinawezekana au hakiwezekani, hiyo siyo hatua hii. Wewe hapa funguka na andika kila aina ya suluhisho unaloweza kufanyia kazi.
Hakikisha unakuwa muwazi na unaandika kila wazo linalokuja kwenye kichwa chako, hata kama litaonekana ni la hovyo au haliwezekani, wewe orodhesha. Ni kwa njia hii ndiyo unaweza kupata njia bora kabisa za kukabiliana na tatizo unalokutana nalo.
Hatua ya tatu; andika faida na hasara za kila suluhisho.
Baada ya kuorodhesha hatua zote unazoweza kuchukua, yaani kila aina ya suluhisho unaloweza kuchukua, sasa unakwenda kuchambua suluhisho moja baada ya jingine.
Andika kila suluhisho na gawa pande mbili, upande mmoja andika faida utakayopata kama utachukua hatua hiyo, na upande wa pili andika hasara za kuchukua hatua hiyo. Andika kila kitu ambacho unafikiria kuhusu suluhisho husika. Na fanya hivi kwa masuluhisho yote uliyoorodhesha kwenye hatua ya pili hapo juu.
Hatua ya nne; chagua suluhisho sahihi.
Baada ya kujua faida na hasara za kila suluhisho, sasa unaweza kuchagua suluhisho sahihi kwako kufanyia kazi. Hapa angalia lile ambalo lina faida kubwa na nzuri na hasara kidogo. Na unapoangalia mambo hayo kuwa makini usifumbwe macho na faida za muda mfupi ambazo mara nyingi zinakuja na hasara za muda mrefu.
Chagua suluhisho ambalo una uhakika unaweza kulifanya na hutokuja kujutia hapo baadaye. Pia hakikisha unaweza kusimamia suluhisho hilo bila ya kutetereka na kuweza kulitetea kwa wengine.
SOMA; Jambo Muhimu Kuzingatia Kabla Ya Kuwasaidia Wengine, Ili Msaada Wako Uwe Bora.
Hatua ya tano; fanya mapitio ya suluhisho ulilochukua.
Ukishachukua hatua siyo mwisho, bali unahitaji kuwa unafanya mapitio na tathmini ya ile hatua uliyochagua kuchukua. Je inaleta matokeo ambayo ulitarajia kupata? Je kuna changamoto nyingine zinaibuka?
Bila ya kufanya tathmini unaweza kushangaa muda unakwenda lakini tatizo linaendelea kuwepo licha ya kupata suluhisho. Unapofanya tathmini unaona ni wapi panahitaji mkazo zaidi na wapi pako vizuri.
Hizo ndizo hatua tano muhimu za kufuata pale unapotaka kutatua tatizo lolote unalokutana nalo. Fuata hatua zote tano kwa mfuatano, usikimbilie hatua ya juu kama ya chini bado hujaikamilisha. Usiwe na haraka, ukishaingia kwenye matatizo unahitaji kutuliza akili yako ndiyo uweze kutatua matatizo hayo.
Kitu kingine muhimu sana kuzingatia ni uvumilivu, usitake kuchukua njia za mkato za kutatua tatizo lolote, maana njia hizi huwa zinaleta matatizo mengine makubwa zaidi.
Fanyia kazi njia hizi tano na kama kuna changamoto zaidi tuwasiliane.
0712562397

Chanzo Kikuu Cha Wivu, Matokeo Yake Na Jinsi Ya Kuondokana Na Wivu.


Habari mpenzi msomaji wetu? Karibu katika makala yetu ya leo ambapo leo tutazungumzia kuhusiana na wivu. Wivu ni nini, ni kitu gani basi mpaka kinapelekea mtu kua na wivu, nini matokeo ya wivu na namna gani au jinsi gani ya kukabiliana na wivu. Wivu ni hali ya kuwa na mtazamo hasi juu ya kitu fulani kwa mfano unachukia au hufurahii kabisa mandeleo ya mwenzako au mtu mwingine anafurahia kuona mwenzake au jirani yake akipatwa na matatizo na wakati mwingine wako watu mpaka wanafurahia misiba ya wenzao.
  Wivu ni hisia ambayo imetawala katika jamii zetu na hisia ambayo inawaumiza watu wengi sana na kuleta athari hasi katika maisha ya mtu mmoja mpaka jamii kwa ujumla. Zifuatazo ni sababu zinazopelekea mtu kuwa na wivu nazo ni;
  1. Kujiona unastahili kuliko wengine; Kujiona wewe ndio unastahili kupata kuliko wengine hiyo inapelekea wivu ukiona mwenzako kapata mafanikio juu ya kitu Fulani unaumia kweli, unapatwa na hasira kabisa na kupata maumivu ya moyo sababu ni kujiona tu wewe ndio unastahili kupata kuliko mtu mwingine. Binadamu wote ni sawa na kila mtu ana haki ya kufanikiwa hivyo hupaswi kujiona kuwa wewe unastahili kupata zaidi kuliko mwingine na ukiwa na zana hii itakutesa sana sehemu yoyote ile ulipo ukiwa kazini kwako mwenzako akipandishwa cheo unapatawa wivu na kujiona kuwa wewe ndio unastahili kuliko wengine. Hivyo kuwa huru na furahia mafanikio ya wenzako na jifunze kupitia wenzako waliofanikiwa badala ya kuonea wivu watu. SOMA; Huyu Ndiye Mtu Anayekuzuia Kufikia Mafanikio Makubwa, Na Jinsi Ya Kumshindwa.
 
2. Kutojiamini; Kutojiamini ni hali ya kujidharau wewe mwenyewe, hali ya kutojiamini inapelekea wivu sehemu mbalimbali. Kwa mfano mfanyakazi anamuonea wivu mfanyakazi mwenzake kwa sababu ya mwenzake anafanya kazi kwa juhudi na maarifa na kuongeza thamani katika kampuni au taasisi yake. Badala ya mfanyakazi mwenzake kuiga mazuri au kujifunza mazuri kutoka kwa mwenzake anaanza kumuonea wivu. Kutojiamini inampelekea kujiona yeye hawezi kuleta mabadiliko katika kampuni au taasisi yake wakati ana kila sababu ya kuwa bora kama mwenzake hivyo basi, hali hii inampelekea mtu wa kutojiamini kuwa na wivu na mwenzake. Wapo watu wengine hawajiamini katika nyadhifa walizonazo au nafasi walizonazo na kupelekea hali ya wivu hata kudiriki kumwendea mwenzake kwa mganga ili aendelee kubaki katika nyadhifa au nafasi aliyopo. Kutojiamini, kutokubali mabadiliko yanayotokea na kutokujifunza zaidi katika taaluma yako na kufanya kazi kwa mazoea bila ubora wowote inapelekea migogoro ya wivu na madhara ya wivu ni makubwa sana katika jamii. 3. Kuishi au Kuzungukwa na Watu Hasi; Kila mtu ana uamuzi wa kuishi maisha anayotaka au aliyojichagulia hivyo kama wewe umezungukwa na watu chanya katika maisha yako uko sehemu nzuri sana ya kufikia mafanikio makubwa. Lakini kama wewe umezungukwa au unaishi na watu hasi upo sehemu mbaya na ya hatari sana. Kuzungukwa na watu hasi ni kama vile kuwa na marafiki, ndugu, majirani wenye mtazamo hasi hata kuzungukwa na watu hasi katika mitandao ya kijamii inapelekea hali ya mtu kuwa na wivu unakuta mtu ameambatana na watu hasi katika mitandao ya kijamii yeye kila siku ni kuingiza umbea, majungu, katika akili yake hali hii inapelekea kujenga dhana ya wivu. SOMA; Kama Unajibebesha Mizigo Hii Katika Maisha Yako, Sahau Kuhusu Mafanikio. Matokeo ya kuwa na wivu ni kama ifuatavyo; i. Kukosa upendo na watu wengine ii. Kutopenda kuona watu wakifurahi iii. Kuishi na nyuso za huzuni iv. Kukosa furaha v. Kupata majeraha ya moyo vi. Kuishi maisha ya chuki vii. Kuishi maisha ya kutokuwa na amani viii. Huleta mauti ix. Huleta msongo wa mawazo x. Kudhoofika kiafya, kama vile kimwili, kiakili na kiroho. Namna gani au jinsi unaweza kukabiliana na wivu? Unaweza kukabiliana na wivu kwa kutumia njia zifutazo nazo ni; i. Usijilinganishe Na Mtu Mwingine; Matatizo ya wivu huanza pale mtu unapoanza kujilinganisha na mtu mwingine. Unajidharau na kujiona maisha yako unayoishi hayana maana na kuona maisha ya mwenzako ndio bora kwa njia hii lazima itakupelekea kwenye wivu tu. Utatamani kitu ambacho hakipo ndani ya uwezo wako matokeo yake mawazo hasi ya yatakutawala na kupelekea hisia za hasira na hatimaye kuwa na wivu. Hii ni dawa namba moja ya kuepukana na wivu usijilinganishe na mtu mwingine na ishi maisha yako. SOMA; Jinsi Unavyoweza Kuwa Sumaku Ya Fedha, Njia Kumi (10) Za Kuivuta Fedha Ije Kwako Muda Wote. ii. Usimdharau Mtu Mwingine; Kila binadamu ameumbwa kwa mfano na sura ya Mungu. Hivyo basi huna haki ya kumhukumu mtu mwingine na kumdharau kulingana na rangi, jinsia, jinsi, maumbile yake na hata ulemavu wowote ule. Mwenye haki ya kuhukumu si wewe bali ni Mungu acha mara moja tabia ya kuhukumu na kudharau wengine. Kama binadamu ameumbwa kwa mfano na sura ya Mungu basi ukimdharau mtu mwenzako utakuwa umemdharau aliyemuumbwa. Hakuna aliyeandika barua ya kuomba kuzaliwa na azaliwe na namna gani bali wote tunatakiwa kujipokea kama tulivyozaliwa na wala tusiwadharau watu wengine. Makala hii imeandikwa na Michael Charles Chali ambaye ni mwanafunzi  mwandishi kutoka Chuo Cha Uandishi wa habari (Dsj), mhamasishaji na mjasiriamali,unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0712562397 au kwa barua pepe micha.connect2015@gmail.com

Huyu Ndiye Adui Namba Moja Kwenye Malezi Ya Watoto.


Habari mpenzi msomaji? 
Karibu katika makala yetu ya leo ambapo tutazungumzia adui namba moja katika malezi ya watoto. Karibu tujifunze kwa pamoja ndugu msomaji. Licha ya changamoto ya kiuchumi kusumbua watu wengi lakini siku hizi malezi kwa watoto imekuwa changamoto miongoni mwa wazazi wengi. Wazazi wengi wamehamia katika ulimwengu wa ‘ubize’ na kusahau wajibu wao katika malezi ya watoto na hatimaye watoto wanakosa malezi mazuri katika familia watoto wanageuka kuwa yatima kama vile hawana wazazi, watoto wanakosa upendo kutoka kwa wazazi wao. Inafikia kipindi watoto wanawaogopa wazazi wao wanaishi maisha kama ya paka na panya maisha ambayo hayana furaha, amani na upendo. 
 
Wewe kama mzazi unapata faraja gani kuwa na mafanikio halafu familia yako ni mbovu? Familia haina amani, furaha na upendo? Wazazi wengine ni wabishi hawataki kukubali kosa kuwa wamekosea ili wabadilike na kuboresha familia zao. ‘Ubize’ wako hauna maana kama umesahau jukumu la malezi ya watoto wenu, wazazi wakishazaa tu wanaachia wasichana wa kazi ndio walee watoto au wengine wanawapeleka watoto kwa bibi zao ili walelewe wao hii sio haki kabisa, jukumu la malezi siyo la bibi na babu au dada wa kazi. Mafanikio yako, ubize wako hauna maana kama familia yako ni mbovu na watoto wako wameharibika kutokana na kukosa malezi bora.
 
SOMA; Mambo Matano(5) Muhimu Ya Kuzingatia Kwenye Malezi Ya Watoto Ili Kuwaandaa Kufikia Mafanikio.
Kwa hiyo, ni dhahiri kabisa adui namba moja katika malezi ya watoto ni mzazi au wazazi. Watoto wanahitaji kupata malezi kutoka kwa baba na mama, mtoto aonje upendo wa wazazi aone thamani ya kuwa na wazazi, acha kusingizia ubize na kutafuta sababu juu ya malezi ya watoto, acha kulea watoto kama vile bata anavyolea watoto wake. Bata anatangulia mbele yeye anawaacha watoto nyuma wala hana habari nao na wazazi wengine kweli wanawalea watoto kama vile bata anavyowalea watoto wao. Mpe malezi mazuri mtoto wako kama vile ndio siku yako ya mwisho hapa duniani, kama hujawahi kumwambia mtoto wako nakupenda mwanangu basi mwambie leo, kama hujawahi kumkumbatia mwanao mkubatie leo, kama hujawahi kumbusu mtoto wako basi mbusu leo afurahie uwepo wa mzazi wake hapa duniani. Changamoto za kidunia zipo lakini zisikufanye ushindwe kumlea mtoto katika malezi mazuri.
Wazazi wakikosa misingi imara na familia inayumba, huwezi kumpata mtu sahihi kama wewe siyo mtu sahihi ukitaka kumpata mtu sahihi basi kuwa sahihi kwanza wewe mwenyewe, ukitaka familia yako iwe bora, iwe sahihi kama wewe ni mzazi basi kuwa bora kwanza wewe na familia itakua bora. Huwezi kuiambia familia iwe bora yaani watoto wakati wewe mzazi siyo bora. Kuwa mfano kwa familia yako nayo itakua bora. Inasikitisha sana pale mzazi anapotengeneza hali ya ubinafsi mfano kuna wazazi wengine wanaangalia Tv chumbani hii ni kukwepa kukaa na watoto na kutengeneza chuki, wazazi mkipata nafasi ya kuangalia tv na watoto kaeni pamoja mzungumze pamoja, mcheke na mfurahi ndio raha ya familia, hata mkipata nafasi ya kula pamoja kuleni pamoja watoto muwaoneshe upendo wa kukaa mezani na kula pamoja siyo ukionana mtoto ni salamu tu na huna muda tena mtoto.
Shida ya malezi inaanza kwa wazazi wenyewe kama wazazi wamekosa kuwa na upendo wao wenyewe wanatengeneza mazingira ya hofu, chuki na visasi katika familia na hatimaye kuwagawa watoto. Watoto wote ni sawa tuwapokee kama tulivyopewa acheni tabia ya kusema mtoto huyu ni wangu na mtoto huyo ni wako wape haki sawa ya malezi watoto wote bila ubaguzi. Kuwapa watoto adhabu kupita kiasi na mtoto kutopewa adhabu akifanya kosa nayo ni hatari katika malezi, kuwapa watoto adhabu mbadala kama vile kumzomea mtoto, kumtukana unamwathiri mtoto kisaikolojia. Watoto wengine wanalelewa malezi ya ajabu katika familia na kufanywa wao ndio watawala wa familia anafanya chochote anachojisikia na mzazi hana kauli juu ya mtoto.
SOMA; Huyu Ndiye Mwalimu Wa Kwanza Na Muhimu Sana Kwenye Malezi Ya Mtoto.
Dawa nzuri ni kubadilika tu kwa wazazi bila kuweka sababu na kujitambua kuwa jukumu la malezi ni la kwako na mtoto akiharibika mzigo unakua ni kwa wazazi hata ukiwa mtafutaji mzuri familia yako ikiwa ni mbovu mali zako zina faida gani? Kulingana na ubize huu unawafanya wazazi hata kuwapeleka watoto wadogo kabisa shule za bweni kwa sababu ya majukumu na kukwepa wajibu wao, ni hatari kwa mtoto kwani unamnyima haki ya malezi yake ambayo hawezi kuipata sehemu nyingine yoyote zaidi ya wewe mzazi. Pia kuwaanzisha watoto shule wakiwa na umri mdogo chini ya miaka 5 wanakadiriwa kuishi maisha mafupi ukilinganisha na watoto wanaoanza shule wakiwa na miaka 6 hii ni kulingana na tafiti zilizofanyika kwa miaka 80 kuanzia mwaka 1921 na ulianzishwa na Dr Terman utafiti huu upo katika kitabu cha The Longevity Project. Pia dini ina mchango mkubwa katika malezi ya watoto hivyo ni wajibu kuwafundisha watoto dini ili wawe na hofu ya Mungu katika maisha yao.
Kwa kuhitimisha makala hii, wazazi ndio kioo katika malezi ya mtoto na ili tuwe na jamii bora lazima tuwe na familia bora na msingi wa familia bora unajengwa na wazazi wawili. Baba na mama wakiyumba na familia nzima inayumba hivyo basi, wazazi wana mchango mkubwa sana katika malezi ya watoto.
Makala hii imeandikwa na Michael Charles Chali  ambaye ni Mwanafunzi mwandishi katika Chuo Cha Uandishi wa habari (Dsj) , mhamasishaji na mjasiriamali, unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0712 562397au kwa barua pepe micha.connect2015@gmail.com

Hivi Ndivyo Watu Wanavyoua Biashara Au Ajira Zao Wenyewe Na Jinsi Ya Kuepuka.


Kama una biashara na ikafa, au umewahi kuwa na biashara siku za nyuma na ikafa, basi kwa sehemu kubwa sana ni wewe mwenyewe uliua biashara yako. na kama kwa sasa una biashara lakini haifanyi vizuri kama ambavyo ulikuwa unategemea, jua ya kwamba wewe mwenyewe ndiyo sababu kubwa ya biashara yako kukwama. Pia kwenye ajira, kama umewahi kuajiriwa lakini kazi ile ikaisha, yaani ukafukuzwa au ukaamua wewe mwenyewe kuacha, basi sehemu kubwa ya kilichokufikisha hapo ni wewe mwenyewe. Na kama kwa sasa upo kwenye ajira lakini unaona kama ajira imedumaa, huoni ukikua na wala kipato chako hakikui, kazi imekuchosha na upo tu, basi kuna mambo unayofanya na yanaelekea kumaliza kabisa ajira yako. Kuna sababu nyingi sana zinazopelekea biashara au ajira kufa. Leo hapa tunakwenda kuangalia sababu moja kubwa sana, ambayo ndiyo imeua biashara na ajira za wengi. Na cha kushangaza sana kuhusu sababu hii ni kwamba inaanza na mtu mwenyewe, na wala haitoki nje ya mtu. Nyoosha mkono kama umewahi kuona hali kama hii; Mtu anaanzisha biashara yake, ana malengo na mipango mikubwa, anakuwa na hamasa kubwa sana. Biashara inaanza, anapata wateja wengi, anakazana sana kuwahudumia, na wanafurahia. Lakini baada ya muda wateja wanaanza kulalamika kwamba zile huduma walizokuwa wanapata zamani sasa hivi hawapati tena, na mmoja mmoja wanaanza kuihama biashara. Na hali hii inapotokea mwenye biashara anakazana kuibadili kwa kuzidi kubana mambo kwenye biashara yake. Au mtu anaajiriwa, mwanzoni anakuwa na hamasa kubwa sana kuhusu ajira yake hiyo. Kwenye usaili aliahidi kwamba atajituma sana kwenye kazi na atafanya kadiri ya uwezo wake kuhakikisha anaongeza thamani. Kazi inaanza na anaweka juhudi kweli, anaongeza thamani. Lakini kadiri muda unavyozidi kwenda mtu anaichoka kazi, anaanza kuona kama juhudi zote anazoweka ni kazi bure, anaanza kuhoji kipato anachopewa na juhudi anazoweka. Kidogo kidogo kazi inapoteza umaarufu kwake, uzalishaji wake unapungua na hatimaye anaacha au kufukuzwa kazi. Hizi ni hadithi ambazo zipo kwa wengi, zinaweza kuwa na utofauti kwenye mtiririko wa matukio lakini mwanzo na mwisho unafanana kabisa Je ni kitu gani kinapelekea hali kama hizi? Matatizo yote haya yanaanzia kwenye eneo moja muhimu sana kwenye biashara au kazi yoyote. Na eneo hili muhimu ni huduma kwa wateja. Watu wengi wanapoingia kwenye biashara na kupata wateja wengi mwanzoni, hujisahau na kufikiri wateja wananunua kwao kwa sababu wapo. Wanasahau kwamba wateja wananunua kwa sababu zao binafsi, kwa sababu wana mahitaji na wamepata wanakoridhishwa nako. Mtu anaposahau au anapokuwa hajui hili muhimu anaanza kuweka mazoea kwenye biashara yake, wateja wanachoka na kutafuta sehemu nyingine ambayo itawatimizia mahitaji yao. Hata kwenye ajira, wengi wanapoajiriwa mwanzoni wanakuwa wakijua kwamba juhudi zao ndiyo mafanikio ya ajira zao. Na hivyo wanaweka juhudi sana, na wanaona matokeo mazuri. Lakini siku zinapokwenda wanaanza kuzoea kazi na kuona wao ni sehemu ya kazi hiyo. Hivyo wanasahau ule msingi muhimu uliowajenga mwanzo na hivyo kuanza kufanya kwa mazoea. Wanapoanza kufanya kwa mazoea wanapunguza uzalishaji wao na wale wanaotegemea kazi zao wanaanza kuacha kuzitegemea. Hii inamuathiri mwajiriwa mwenyewe na hata mwajiri wake. Inapotokea kwamba kuna mtu mwingine wa kuzalisha vizuri kuliko aliyepo, basi nafasi inakwenda kwake. Jim Rohn, aliyekuwa mwandishi na mhamasishaji kutoka marekani alikuwa akisisitiza sana hili; unalipwa kulingana na thamani unayopeleka sokoni. Kwa lugha rahisi ni kwamba unalipwa kulingana na thamani unayompatia mteja wako. Iwe ni kwenye biashara au kwenye ajira, kipimo pekee cha malipo yako ni je mteja amenufaikaje na kile ulichofanya? Kwa sababu ni mteja ndiye anayelipa na sehemu ya faida inakuja kwako, iwe ni kwenye biashara yako binafsi au kwenye ajira. Bila ya mteja hakuna biashara na wala hakuna kazi. Ndiyo maana mteja ni sehemu muhimu sana ya biashara yoyote au kiwanda chochote kinachozalisha, au taasisi yoyote inayotoa huduma zake kwa watu. Ufanye nini ili kuepuka kuua biashara au ajira yako mwenyewe? Kama tulivyoona ya kwamba mteja ndiyo nguzo muhimu ya mafanikio kwenye biashara au kazi, basi ni muhimu sana wewe kuwa na maarifa sahihi juu ya utoaji wa huduma bora sana kwa wateja wako. Hili ni eneo ambalo watu wengi huwa hawajifunzi na kuishia kufanya tu kwa mazoea. Mazoea haya yamekuwa yakiathiri sana biashara na hata kazi zao. Amka Consultants tumekuandalia semina ya UTOAJI WA HUDUMA BORA SANA KWA WATEJA. Semina hii itaendeshwa kwa njia ya mtandao hivyo unaweza kushiriki popote pale ulipo. Semina itaanza tarehe 02/05/2016 na itaendeshwa kwa siku kumi. Kwenye semina hii utajifunza haya yafuatayo; 1. Kila mtu anauza, je wewe unauza nini? 2. Nani ni mteja wako? 3. Mahitaji ya msingi ya mteja wako. 4. Jinsi ya kutatua hali ya kutoelewana baina yako na mteja wako. 5. Mfanye mteja kuwa rafiki yako. 6. pokea maoni ya wateja wako. 7. Kitu kimoja unachotakiwa kuzingatia sana na kitakunufaisha wewe na mteja wako. 8. Gharama za huduma mbovu kwa wateja wako. 9. Vaa viatu vya mteja wako. 10. Matumizi ya mtandao na teknolojia katika kuboresha huduma kwa wateja. Karibu sana ushiriki semina hii ambayo itakupa mbinu bora za kutoa huduma bora kwa wateja wako na hivyo kuendelea kufanikiwa kwenye biashara na kazi yako. kushiriki semina hii tuma ada ya ushiriki ambayo ni tsh elfu 20 (20,000/=) kwenye namba zifuatazo; tigo pesa 0712562397 namba zote jina Michael Charles . Baada ya kufanya malipo tuma ujumbe kwenye moja ya namba hizo au tuma ujumbe kwa wasap kwenye namba 0712562397. Pia bonyeza maandishi haya na jaza taarifa zako. Ni wakati sasa wa kuongeza umakini kwenye biashara na kazi yako ili uweze kufikia mafanikio makubwa zaidi. Karibu tujifunze kwa pamoja.

Kama Una Tabia Hii Moja Una Uhakika wa Zaidi ya 90% Wa Kufanikiwa Kwenye Chochote Unachofanya.


Kuna tabia moja muhimu sana ambayo inaonekana kwa watu waliofanikiwa sana kwenye kila nyanja ya maisha. Tabia hii kuna watu wengi wanayo ila hawajajijua na kuanza kuitumia na hata kama huna unaweza kuiendeleza na wewe ukafanikiwa sana kwenye maisha yako. Kabla ya kuiangalia tabia hiyo hebu kwanza tuone tafiti zilizofanywa kudhibitisha uhusiano wa tabia hii na mafanikio.
  Miaka ya 1960 profesa Walter Mischel wa chuo kikuu cha Stanford, alianza kufanya tafiti zilizodumu kwa miaka 40 kuhusiana na tabia hii. Katika utafiti wake aliwahusisha watoto wadogo wenye miaka minne mpaka mitano na kugundua siri moja muhimu kwenye mafanikio ya kazi, biashara, afya na maisha kwa ujumla.
  Utafiti huu ulihusisha pipi tamu iliyotengenezwa kwa asali na mmea ijulikanayo kama marshmallow, pipi hii hupendwa sana na watoto.
Katika utafiti huu kila mtoto aliwekwa kwenye chumba chake mwenyewe na mtafiti alileta pipi hiyo aina ya marshmallow. Aliweka pipi hiyo mbele ya mtoto na kumwambia yeye anaondoka na atarudi baadae. Kama akirudi akakuta mtoto hajala hiyo pipi atamuongezea pipi nyingine, ila akikuta ameshakula hatamwongezea nyingine. Kwa hiyo uchaguzi ulikuwa ni kula moja sasa au kusubiri ule mbili baadae.
  Mtafiti aliondoka kwa dakika kumi na tano. Kuna watoto walikula pipi zao mara moja, wengine walijaribu kujizuia ila wakashindwa na wachache sana waliweza kusubiri wasile pipi zao mpaka mtafiti aliporudi. Majibu ya utafiti huu yalitolewa mwaka 1972, kitu kikubwa cha kushangaza kilitokea miaka 40 baada ya utafiti huu.
marshmallowmarshmallow2
  Watafiti waliendelea kuwafuatilia watoto hawa mwaka hadi mwaka kwa kipindi cha miaka 40. Katika ufuatiliaji iligundulika kwamba watoto waliojizuia kula pipi na kusubiri mtafiti arudi, walikuwa na ufaulu mkubwa darasani, walikuwa na uwezekano mdogo wa kutumia mihadarati na waliweza kukabiliana vizuri na changamoto mbalimbali.
  Kwa miaka 40 ya ufuatiliaji mpaka wanakuwa watu wazima, wale ambao waliweza kusubiri na kutokula pipi walikuwa wamefanikiwa sana ukilinganisha na wenzao walioshindwa kuvumilia. Walikuwa na vipato vizuri, afya njema, familia nzuri na mengine mengi kwenye maisha.
  Katika utafiti huu inaonesha kwamba wale wenye uwezo wa kuvumulia na kuepuka furaha ya haraka ili kupata furaha kubwa zaidi baadae wana uwezekano mkubwa wa kufanikiwa kuliko ambao hawana tabia hiyo.
  Hii ni dhahiri kabisa kwenye maisha yetu ya kila siku, wale ambao wanashindwa kuzuia tamaa zao za kupata furaha ya haraka wanajikuta wanashindwa kufanikiwa sana kwenye maisha.
Kama ukiweza kuepuka tamaa ya kufanya starehe utakuwa na muda mwingi wa kufanya shughuli zako na kuwa na matumizi mazuri ya fedha zako. Kama utaepuka tamaa ya kula vyakula vilivyoandaliwa haraka kama chips utakuwa na afya bora. Kama utaepuka tamaa ya kuangalia tv au movie ambavyo vinakupa starehe ya muda mfupi utakuwa na muda mwingi wa kujifunza vitu vya ziada ambavyo vitakusaidia sana kwenye maisha yako.
  Kwenye maisha ya kila siku tunaona ni jinsi gani watu wenye tamaa ya furaha ya muda mfupi wanavyoharibu maisha yao. Wengi wao wanakuwa wezi, walevi, waasherati na masikini wa muda mrefu.
Je unawezaje kutengeneza tabia hii?
Kama mara nyingi umekuwa ukichagua njia rahisi ya kupata furaha inaonesha kwamba tayari haupo kwenye njia ya kupata mafanikio. Je tabia hii ya kuzuia furaha ya muda mfupi ni ya kuzaliwa? Watoto hao walioweza kujizuia kula pipi walizaliwa na tabia hiyo? Je wewe unawezaje kujifunza tabia hii ili uweze kufanikiwa?
  Kabla ya kujibu maswali haya hebu twende kwenye sehemu ya pili ya utafiti huu ambao una majibu mazuri na ya kushangaza kidogo.
Endelea kusoma tabia hii kwenye KISIMA CHA MAARIFA.

Hivi Ndivyo Unavyoweza Kutajirika Kwa Kuanza Na Shilingi Elfu Moja.


Moja ya sababu kubwa ambayo watu wengi husema kwamba inawazuia kufanya biashara ni mtaji. Mimi huwa nakataa sana sababu hii kwa sababu haiwezekani leo huna mtaji, mwaka kesho huna mtaji na hata miaka mitano ijayo huna mtaji. Nasema mtaji ni kigezo tu ambacho watu wengi hutumia kuficha sababu halisi ya kutokuingia kwenye biashara ambayo ni kutokujipanga na kutokuwa tayari.
Leo nakushirikisha siri moja ambayo itakuwezesha kufikia mafanikio makubwa sana japo utaanza kidogo. Kupitia siri hii unaweza kuanza na tsh elfu moja na baadae ukapata mtaji ambao utakuwezesha kufanya biashara kubwa. Pia tutaangalia kama ukianza na kiasi kikubwa kidogo itakavyokuwa bora zaidi.

ANGALIZO; Mambo utakayoyasoma hapa yatabadili kabisa maisha yako kama ukiyatumia. Ila kama utayasoma na kupita utaendelea kuwa na maisha magumu huku ukilalamika bila ya msaada wowote. Hivyo chukua hatua, huu ndio ukombozi wako.
Siri kubwa nitakayoizungumzia hapa ni kuweka akiba kidogo kidogo kila siku na kwa muda mrefu ili kuweza kuondoka kwenye tatizo la fedha uliloko nalo sasa. Na akiba hii hitaiweka benki ambako utawafaidisha sana na hela yako kuliwa na mfumuko wa bei, bali utaiweka kwenye mfuko wa dhamana ambao una uhakika wa kukua kwa asilimia sio chini ya kumi kwa mwaka. Mfano wa mfuko wa dhamana ni Umoja Fund wa UTT(Unit Trust of Tanzania) maarufu kama mfuko wa umoja au vipande vya umoja.
Kupitia mfuko huu unanunua vipande ambavyo vinakua kwa thamani kadiri muda unavyokwenda. Kwa mwaka vinakua sio chini ya asilimia kumi na mara nyingi inakuwa zaidi ya hapo. Hivyo hii ni njia nzuri sana ya wewe kukuza mtaji wako hata kama unaanzia sifuri.
Sasa tuone maajabu ya kuweka fedha kwa muda mrefu.
1. Kama utaanza kuweka tsh elfu moja kwa siku.
Naamini kama unasoma hapa huwezi kukosa tsh elfu moja kila siku. Hata uwe ni mmachinga, mama ntilie, au mpiga debe unaweza kupata tsh elfu moja kila siku. Usiidharau elfu moja hiyo maana ni njia yako ya kuelekea kwenye utajiri.
Kama kila siku utaweka tsh elfu moja, kwa mwezi itakuwa tsh elfu 30, kwa mwaka itakuwa tsh 360,000/=. Kama utaweka fedha hii kwenye mfuko unaokua kwa asilimia 10 kwa mwaka, kwa miaka mitano itakuwa tsh 2,997,403.20 hii ni sawa na tsh milioni tatu. Hiki ni kiasi ambacho huenda hujawahi kukipata kutoka kwenye vyanzo vyako mwenyewe ndani ya miaka mitano iliyopita.
Kama utaweka elfu moja hiyo kila siku kwa miaka kumi itakuwa tsh 7,244,967.43, milioni saba ni fedha ambayo huenda hujawahi kuota kuishika.
Kama bado ni kijana na ukaiweka fedha hii kwa miaka 20 itakuwa tsh 25,102,799.78(milioni 25) na ukiiweka kwa miaka 30 itakuwa tsh 71,421,417.80(milioni 71). Yaani kama wewe una miaka 35 au chini ya hapo, kama utaanza kuweka tsh elfu moja kila siku na ukaiweka fedha hii kwenye mfuko wa umoja utakapokuwa na miaka 60 utakuwa na tsh milioni sabini.
compound
2. Kama utaanza na tsh elfu hamsini kwa mwezi.
Kama unafanya kazi ila una mshahara kidogo sana bado unaweza kujikusanya na kupata mtaji wa kutosha kukuondoa hapo ulipo. Kwa mfano kama mshahara wako uko kati ya laki mbili mpaka laki tano, kwa njia yoyote ile unaweza kujikaza na ukaweka pembeni tsh elfu 50 kila mwezi. Kama fedha hii utaiweka kwenye mfuko wa umoja, kwa miaka mitano itakuwa tsh 4,995,672.00(milioni 5), miaka kumi tsh 12,074,945.71, miaka 20 tsh 41,837,999.64 na miaka 30 tsh 119,035,696.34. Milioni tano kwa miaka mitano, 12 kwa miaka kumi, 41 kwa miaka 20 na 119 kwa miaka 30 ni fedha ambazo unaweza kuanzia nazo na ukafanya mabadiliko makubwa kwenye maisha yako.
3. Kama utaanza na laki moja kwa mwezi.
Kama unafanya kazi na mshahara wako ni kati ya laki tano na milioni moja kwa mwezi, unaweza kujibana na kuweka pembeni tsh laki moja kila mwezi. Kama utaiweka fedha hii kwenye mfuko wa umoja unaokua kwa asilimia 10 kwa mwaka mambo yatakuwa hivi; Miaka mitano tsh 9,991,344.00(milioni 10), miaka 10 tsh 24,149,891.43, miaka 20 tsh 83,675,999.27 na miaka 30 tsh 238,071,392.67. Milioni kumi kwa miaka 5, 24 kwa miaka 10, 83 kwa miaka 20 na hata milioni mia mbili na arobaini kwa miaka 30 ni fedha ambayo inaweza kubadili kabisa maisha yako kama utaanza kuweka tsh laki moja kila mwezi.
Hii ndio siri kubwa ninayokushirikisha leo na kama utaanza kuitumia leo, namaanisha leo hii utaona mabadiliko makubwa sana. Kama usipoitumia naomba unitafute tarehe 10/10/2019 (miaka mitano ijayo) na uniambie ni kipi kikubwa ulichofanya. Miaka mitano sio mingi kabisa rafiki yangu, kama unafikiri ni mingi kumbuka ni lini ulifanya uchaguzi mkuu na mwaka kesho ni uchaguzi mwingine.
Hoja yangu kubwa ni kwamba kama umeweza kuteseka kwenye kazi kwa miaka zaidi ya kumi na huoni mabadiliko makubwa kwa nini usijipe miaka kitano tu au kumi tu na uweke kiasi fulani cha akiba na baada ya hapo upate mtaji wa kuanzia?
Na katika miaka hii mitano au kumi ambayo mtaji wako unakua na unaendelea kuuweka, jifunze kuhusu biashara unayotaka kufanya. Jifunze kwa kujisomea, jifunze kwa kufanya utafiti na pia jifunze kwa kufanya kazi inayohusiana na biashara unayotaka kuja kufanya. Kama kila siku kwamiaka motano au kumi utajifunza kuhusiana na kitu unachotaka kufanya utaona fursa nyingi sana za wewe kutoka.
Uanzie wapi?
1. Leo hii nenda katika ofisi za UTT(kama upo dar nenda sukari house ghorofa ya kwanza, unaweza kutembelea tovuti yao www.utt-tz.com), jiandikishe kuwa mwanachama na watakupa utaratibu wa kuwa unatuma fedha zako hata kwa mpesa, hivyo huna haja ya kwenda benk au ofisini kila mara. Ukisema unasubiri jumatatu au mwisho wa mwezi tayari fursa hii imekupita, na miaka mitano ijayo utajuta sana.
2. Baada ya hapo weka tsh elfu moja pembeni kila siku, unaweza kuwa unaiweka kwenye mpesa halafu kila mwisho wa mwezi unatuma UTT tsh elfu 30. Pia unaweza kutuma zaidi ya hapo kulingana na mipango yako, hiyo 30 kwa mwezi ni kiwango cha chini ambacho kila mtu ambaye yuko makini na maisha yake anaweza kukiweka. Kama unataka kuweka kiwango tofauti na nilivyotumia hapo juu au kwa miaka tofauti bonyeza maandishi haya na utakuta fomula niliyotumia.
3. Wakati unaendelea kuweka fedha hizi na kuzikuza endelea kujifunza kuhusiana na biashara unayotaka kufanya. Unaweza kukaribia kwenye kundi letu la TANZANIA VORACIOUS READERS ambapo tunapanga kusoma vitabu 500 kwa miaka mitano(nitumie email kujua zaidi kuhusu kundi hilo,  Kama kwa miaka hii 5 utasoma vitabu 500 na wakati huo unaendelea kukuza mtaji, mambo yataanz akufunguka kabla hata hujafika miaka hiyo mitano.
Chukua hatua sasa hivi, kama unafikiri haiwezekani kaendelee kulalamika. Kama umechoka kulalamika huu ndio wakati wa kushika hatamu ya maisha yako.
Nakutakia kila la kheri katika safari yako ya kufikia mafanikio makubwa.
TUKO PAMOJA.