Kama una biashara na ikafa, au umewahi kuwa na biashara siku za
nyuma na ikafa, basi kwa sehemu kubwa sana ni wewe mwenyewe uliua biashara yako.
na kama kwa sasa una biashara lakini haifanyi vizuri kama ambavyo ulikuwa
unategemea, jua ya kwamba wewe mwenyewe ndiyo sababu kubwa ya biashara yako
kukwama.
Pia kwenye ajira, kama umewahi kuajiriwa lakini kazi ile
ikaisha, yaani ukafukuzwa au ukaamua wewe mwenyewe kuacha, basi sehemu kubwa ya
kilichokufikisha hapo ni wewe mwenyewe. Na kama kwa sasa upo kwenye ajira lakini
unaona kama ajira imedumaa, huoni ukikua na wala kipato chako hakikui, kazi
imekuchosha na upo tu, basi kuna mambo unayofanya na yanaelekea kumaliza kabisa
ajira yako.
Kuna sababu nyingi sana zinazopelekea biashara au ajira kufa.
Leo hapa tunakwenda kuangalia sababu moja kubwa sana, ambayo ndiyo imeua
biashara na ajira za wengi. Na cha kushangaza sana kuhusu sababu hii ni kwamba
inaanza na mtu mwenyewe, na wala haitoki nje ya mtu.
Nyoosha mkono kama umewahi kuona hali kama hii;
Mtu anaanzisha biashara yake, ana malengo na mipango mikubwa,
anakuwa na hamasa kubwa sana. Biashara inaanza, anapata wateja wengi, anakazana
sana kuwahudumia, na wanafurahia. Lakini baada ya muda wateja wanaanza
kulalamika kwamba zile huduma walizokuwa wanapata zamani sasa hivi hawapati
tena, na mmoja mmoja wanaanza kuihama biashara. Na hali hii inapotokea mwenye
biashara anakazana kuibadili kwa kuzidi kubana mambo kwenye biashara
yake.
Au mtu anaajiriwa, mwanzoni anakuwa na hamasa kubwa sana kuhusu
ajira yake hiyo. Kwenye usaili aliahidi kwamba atajituma sana kwenye kazi na
atafanya kadiri ya uwezo wake kuhakikisha anaongeza thamani. Kazi inaanza na
anaweka juhudi kweli, anaongeza thamani. Lakini kadiri muda unavyozidi kwenda
mtu anaichoka kazi, anaanza kuona kama juhudi zote anazoweka ni kazi bure,
anaanza kuhoji kipato anachopewa na juhudi anazoweka. Kidogo kidogo kazi
inapoteza umaarufu kwake, uzalishaji wake unapungua na hatimaye anaacha au
kufukuzwa kazi.
Hizi ni hadithi ambazo zipo kwa wengi, zinaweza kuwa na utofauti
kwenye mtiririko wa matukio lakini mwanzo na mwisho unafanana kabisa
Je ni kitu gani kinapelekea hali kama hizi?
Matatizo yote haya yanaanzia kwenye eneo moja muhimu sana kwenye
biashara au kazi yoyote. Na eneo hili muhimu ni huduma kwa wateja. Watu wengi
wanapoingia kwenye biashara na kupata wateja wengi mwanzoni, hujisahau na
kufikiri wateja wananunua kwao kwa sababu wapo. Wanasahau kwamba wateja
wananunua kwa sababu zao binafsi, kwa sababu wana mahitaji na wamepata
wanakoridhishwa nako. Mtu anaposahau au anapokuwa hajui hili muhimu anaanza
kuweka mazoea kwenye biashara yake, wateja wanachoka na kutafuta sehemu nyingine
ambayo itawatimizia mahitaji yao.
Hata kwenye ajira, wengi wanapoajiriwa mwanzoni wanakuwa wakijua
kwamba juhudi zao ndiyo mafanikio ya ajira zao. Na hivyo wanaweka juhudi sana,
na wanaona matokeo mazuri. Lakini siku zinapokwenda wanaanza kuzoea kazi na
kuona wao ni sehemu ya kazi hiyo. Hivyo wanasahau ule msingi muhimu uliowajenga
mwanzo na hivyo kuanza kufanya kwa mazoea. Wanapoanza kufanya kwa mazoea
wanapunguza uzalishaji wao na wale wanaotegemea kazi zao wanaanza kuacha
kuzitegemea. Hii inamuathiri mwajiriwa mwenyewe na hata mwajiri wake. Inapotokea
kwamba kuna mtu mwingine wa kuzalisha vizuri kuliko aliyepo, basi nafasi
inakwenda kwake.
Jim Rohn, aliyekuwa mwandishi na mhamasishaji kutoka marekani
alikuwa akisisitiza sana hili; unalipwa kulingana na thamani unayopeleka
sokoni. Kwa lugha rahisi ni kwamba unalipwa kulingana na thamani
unayompatia mteja wako. Iwe ni kwenye biashara au kwenye ajira, kipimo pekee cha
malipo yako ni je mteja amenufaikaje na kile ulichofanya? Kwa sababu ni mteja
ndiye anayelipa na sehemu ya faida inakuja kwako, iwe ni kwenye biashara yako
binafsi au kwenye ajira.
Bila ya mteja hakuna biashara na wala hakuna kazi. Ndiyo maana
mteja ni sehemu muhimu sana ya biashara yoyote au kiwanda chochote
kinachozalisha, au taasisi yoyote inayotoa huduma zake kwa watu.
Ufanye nini ili kuepuka kuua biashara au ajira yako
mwenyewe?
Kama tulivyoona ya kwamba mteja ndiyo nguzo muhimu ya mafanikio
kwenye biashara au kazi, basi ni muhimu sana wewe kuwa na maarifa sahihi juu ya
utoaji wa huduma bora sana kwa wateja wako. Hili ni eneo ambalo watu wengi huwa
hawajifunzi na kuishia kufanya tu kwa mazoea. Mazoea haya yamekuwa yakiathiri
sana biashara na hata kazi zao.
Amka Consultants tumekuandalia semina ya UTOAJI WA HUDUMA BORA
SANA KWA WATEJA. Semina hii itaendeshwa kwa njia ya mtandao hivyo unaweza
kushiriki popote pale ulipo. Semina itaanza tarehe 02/05/2016 na itaendeshwa kwa
siku kumi. Kwenye semina hii utajifunza haya yafuatayo;
1. Kila mtu anauza, je wewe unauza nini?
2. Nani ni mteja wako?
3. Mahitaji ya msingi ya mteja wako.
4. Jinsi ya kutatua hali ya kutoelewana baina yako na mteja
wako.
5. Mfanye mteja kuwa rafiki yako.
6. pokea maoni ya wateja wako.
7. Kitu kimoja unachotakiwa kuzingatia sana na kitakunufaisha
wewe na mteja wako.
8. Gharama za huduma mbovu kwa wateja wako.
9. Vaa viatu vya mteja wako.
10. Matumizi ya mtandao na teknolojia katika kuboresha huduma
kwa wateja.
Karibu sana ushiriki semina hii ambayo itakupa mbinu bora za
kutoa huduma bora kwa wateja wako na hivyo kuendelea kufanikiwa kwenye biashara
na kazi yako. kushiriki semina hii tuma ada ya ushiriki ambayo ni tsh elfu 20
(20,000/=) kwenye namba zifuatazo; tigo pesa 0712562397
namba zote jina Michael Charles . Baada ya kufanya malipo tuma ujumbe kwenye
moja ya namba hizo au tuma ujumbe kwa wasap kwenye namba 0712562397. Pia
bonyeza maandishi
haya na jaza taarifa zako.
Ni wakati sasa wa kuongeza umakini kwenye biashara na kazi yako
ili uweze kufikia mafanikio makubwa zaidi. Karibu tujifunze kwa pamoja.
No comments:
Post a Comment