Habari rafiki na mpenzi msomaji wetu ,
naamini umzima afya na unaendelea
na harakati za kuboresha maisha yako. Karibu tena katika siku nyingine ya
kujifunza na kuboresha maisha yetu kama ilivyo kawaida yetu. Hili ni jukumu
ambalo unatakiwa kuliendeleza karibu kila siku katika maisha yako.
Kumbuka,
kama ambavyo tumekuwa tukisema mara kwa mara kupitia mtandao huu wa Official Michael Charles Jornalist ni muhimu na ni lazima kuwa
bora zaidi ili kujihakikishia mafanikio ya kudumu. Kwa wale wasomaji wazuri waOfficial Michael Charles Jornalist wanalijua hili vizuri na umuhimu wa falsa ya kuwa bora kila siku
katika maisha yetu.
Na
katika kuhakikisha hili linafanikiwa huwa yapo mambo ambayo tunatakiwa
tujifunze na kuyafanyia kazi kila siku. Mambo hayo, ambayo unatakiwa uyaelewe
na kuyafanyia kazi ili uwe bora siku zote, baadhi tunakwenda kujifunza kupitia makala
hii. Je, ni mambo gani yatakayokufanya uzidi kuwa bora na mafanikio makubwa?
Yafutayo
Ni Mambo 6 Yatakayokufanya Uzidi Kuwa Bora
Na Mwenye Mafanikio Makubwa.
1. Jielewe mwenyewe.
Hatua
mojawapo kubwa itakufanya uzidi kuwaa bora siki hadi siku ni wewe kujitambua
kwanza. Kwa kujijua wewe itakusaidia kujua udhaifu wako na kuboresha yale
maeneo ambayo kwako unaona yana shida au yana kukwamisha kwa kiasi fulani. Watu
wengi huwa wanakwama au kuchelewa kufanikiwa kwa sababu ya kushindwa kujitambua
wao mapema na yale mambo yanayo wakwamisha kufikia mafanikio hayo.
USHINDI NI LAZIMA UKIWA BORA SIKU ZOTE |
2. Kuwa na mawazo chanya.
Maisha
yako yatakuwa bora zaidi na ya wepesi kama utakuwa mtu wa mawazo chanya.
Kinyume cha hapo utageuza maisha yako kuwa mzigo mkubwa ambao utashindwa
kuubeba. Hii ndiyo siri mojawapo pia ya kukufanya uzidi kuwa bora kwa kile unachokifanya.
Hivyo, chochote unachokifanya kitazame kwa mtazamo chanya, hiyo itakusaidia
kuwa bora sana.
3. Kuwa wewe kama wewe.
Utazidi
kujihakikishia ubora mkubwa katika maisha yako ikiwa utabaki kuwa wewe kama wewe. Hakuna mafanikio makubwa
yanayoweza kupatikana kwa kuiga. Kumbuka umeumbwa ukiwa wewe kama wewe, hivyo
kwa kila unalolifanya acha kuiga sana. Jifunze kuwa wewe kama wewe, kwani kuiga
kuna mipaka yake. Ukifanikiwa kumudu hili itakusaidia sana kuwa bora kwenye
maisha yako kuliko unavyofikiri.
4. Jiamini.
Siri
kubwa ya mafanikio ipo kwenye kujiamini. Mipango na malengo mengi yanashindwa
kufanikiwa kwa sababu ya kutokujiamini. Kwa kadri utakavyoweza kujenga nguvu
kubwa ya kujiamini itakusaidia sana kuwa bora wakati wote na kuweza kufikia
mafanikio makubwa ambayo unayahitaji katika maisha yako. Kwa kujiamini tu,
itakusaidia kufikia mafanikio makubwa na kuwa bora zaidi kwenye maisha yako.
5. Kujifunza.
Hitaji
la kwanza ambalo litafanya maisha yako yazidi kuwa bora ni kujisomea kila siku.
Unatakiwa kujifunza kupitia vitabu, semina au mitandao ya kuhamsisha kama iliyo
chini ya Official Michael Charles Jornalist . Kwa bahati mbaya sana tatizo kubwa walilonalo watanzania
wengi ni kule kushindwa kujisomea. Wengi hawapo tayari kupata maarifa haya.
Kama wewe ni mtu wa kujisomea elewa utakuwa umeachana na kundi kubwa na kufuata
njia ambayo itakupeleka kwenye ubora
siku hadi siku.
6. Kuwa msikilizaji mzuri.
Siku
zote acha kuzungumza tu, kama unataka kuwa bora jifunze kuwa msikilizaji mzuri
pia. Unapokuwa msikilizaji inakusaidia kujua mambo mengi ambayo hapo mwanzo
hukuyajua kabisa. kumbuka hata watu wenye mafaniko ni wasikilizaji pia wazuri.
Yapo
mambo mengi ambayo yanaweza kukufanya ukawa bora zaidi. Chukua hatua kwa kwa
kuyafanyaia kazi hayo ili kufikia mafanikio
yako makubwa.
Endelea
kutembelea Official Michael Charles Jornalist
No comments:
Post a Comment