Ni mara nyingi katika maisha
yako umewahi kusikia au kuona watu ambao ni waongeaji sana wazuri wa mipango na
malengo yao. Watu hawa wanapokuwa wanaongelea mipango, mikakati na malengo yao kwa
hakika ni mipango mizuri ambayo ikiwekwa kwenye vitendo ni lazima kufanikiwa
kuwepo.
Lakini pamoja na kuwa na
mipango hiyo mizuri ambayo huwa ina uwezo wa kuwatoa watu hao hata kwenye
umaskini unaowazunguka kwa bahati mbaya sana watu hao huwa siyo watekelezaji wa
mipango hiyo mizuri hujikuta ni watu
kuongea tu bila kufanya kitu chochote. Hawa ni watu ambao tunao karibu kila
siku na tunawajua.
Sasa kitu cha kujiuliza kwa
nini watu hawa, mara nyingi huwa ni waongeaji tu bila kutekeleza kitu chochote.
Kwa kawaida huwa yapo mambo yanasababisha kwa namna moja au nyingine na
kujikuta wakiwa ni watu ambao hawafanyi kitu katika maisha yao. Sababu hizo
huwa ni kama zifuatazo:-
1.
Kutaka kujionyesha.
Wengi wa watu hawa kwa
kutaka kwao sifa, na kujiona wako juu kimaisha mwisho hujikuta ni watu wa kuongelea sana mipango yao bila
kuitekeleza. Hiyo yote huja ili wao kutaka kuonekana kuwa ni watu wa hadhi fulani
kumbe sivyo ndivyo. Kwa kadri utakavyojikuta unataka kujionyesha, elewa ndivyo
ambavyo utendaji wako utapungua.
Kama unataka kufanikiwa,
acha tabia hii mara moja. Maisha yako yanatataka yaonekane katika uhalisia wake
na sio kupanga tu bila utekelezaji. Kwa kujifunza na kulijua hili unatakiwa
kubadili mwelekeo mara moja na sifa zote kuweka pembeni.
2.
Kutokutaka kuwajibika.
Ni kweli hiki ni kitu
ambacho kinawafanya watu hawa wawe ni
watu wa kuongea kutokana na wao kutokutaka kuwajibika. Kutokana na hili la ktokupenda
kuwajibika ama kujituma hujikuta ni watu ambao wanahamishia nguvu zao nyingi
kwenye kuongea badala ya kutenda. Jaribu kuwachunguza wengi utawagundua wako
hivi.
Hawa huwa ni watu wanaopenda
sana kuonekan ni wasomi na wanajua kila kitu. Kwa sababu ya hiyo wanakuwa ni
watu ambao hawawezi kuwajibika ipasavyo na hujikita kwa kushindwa kwao
kuwajibika wanakuwa ni watu wa kushindwa kufanya mambo yatakayoweza kuwaletea
mabadliko katika maisha yao.
3.
Wanasahau mawazo yao mapema.
Pamoja na kuwa watu hawa
huwa ni mafundi sana wa kuongea juu ya ndoto zao lakini huwa ni watu wa kusashau
sana kile walichokiongea. Na hii huwa inatokea kutokana na wao kutoweza
kuyaandika mawazo yao muhimu. Kwa kutokuyaandika mawazo muhimu ambayo
wanatakiwa kuyatekeleza ndivyo hujikuta kubaki kuwa waongeaji.
Ili uweze kusonga mbele na
kubadili maisha yako ikiwa unajua wewe ni mwongeaji unalazimika sana kuandika
mawazo yako muhimu. Kitendo cha kuweza kuandika mawazo muhimu kutakusaidia
kukupa hamasa ya kuweza kuzidi kuendelea tofauti na unavyo ongeongea tu, mwisho
wa siku utajikuta unabaki kuwa mtu wa kuongea tu.
4.
Kukosa hamasa kubwa ya kusonga mbele.
Mara nyingi watu hawa pamoja
na kuongea sana lakini huwa ni watu ambao wanakosa hamasa ya kusonga mbele. Kwa
nini kitu hiki huwa kinatokea? Hii huwa ni kwa sababu wanakuwa ni waongeaji wao
sana kiasi cha kwamba wanajikuta kushindwa kupata ule muda wa kujifunza kwa
wengine mambo ya kimafanikio ambayo yanaweza kuwapa hamasa zaidi, huku wakiamini
wao wanaweza.
Kutokana na kushindwa kupata
muda wa kujifunza kutoka kwa wengine hamasa ya kutenda au kiutendaji kwao
hupungua kidogo kidogo na mwisho wa siku hupotea kabisa. Ili kuweza watu hawa
kusonga mbele na kuwa watendaji ni lazima wajifunze vitu vipya kwa wengine.
Elewa kuwa, kama utazidi
kuwa mwongeaji katika mambo yako sana kuliko utendaji ndivyo unavyofanya maisha
yako kuwa magumu na kuyarudisha nyuma. Ni vizuri kulielewa hilo, vinginevyo
itakuwa ni ngumu sana kwako kuweza kufanikiwa katika maisha yako.
Kwa makala nyingine nzuri
hakikisha unatembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza zaidi.
Tunakutakia kila la
kheri katika safari yako ya mafanikio iwe ya ushindi na endelea kutembelea Official Michael Charles Journalist kwa kujifunza na kuhamasika kila siku, karibu.
No comments:
Post a Comment