Tumeona jinsi ya kuchukua mazoezi ya kuboresha dhana
ya kujiheshimu au nidhamu binafsi katika makala iliyopita.
Kwa kukukumbusha:
Nidhamu
binafsi au dhana ya kujiheshimu ni ile hali ya kufanya kile kizuri unachopaswa
kukifanya kwa kujilazimisha kukifanya ukijitahidi kupingana na uvivu na mambo
yanayokusababisha usikifanye.
Moja ya ujuzi wenye umuhimu na thamani kubwa sana
ambao kila mtu anapaswa awe nao ni nidhamu binafsi. Ni ujuzi ambao unahitajika
katika kila kona ya maisha yako. Wengi hawajui umuhimu wa hii na ndio maana
wachache sana hufanyia kazi kutia nguvu nidhamu hii.
Kinyume cha imani ya kawaida, nidhamu binafsi siyo
tabia ya kujibana, kujinyima uhuru fulani. Inaongeza chembechembe za kujidhibiti,
akili na uvumilivu katika maisha yako. Hii ina maana kuwa itakufanya uwe na
uwezo mkubwa wa udhibiti wa mambo kadha katika maisha yako.
Nidhamu binafsi inakupa nguvu za kudumu katika
uamuzi wako na kuufuata, bil akubadilisha uamuzi wako na kuyumbayumba, na hivyo
hii ni moja ya zana muhimu sana katika ufanikishaji wa malengo.
Kuwa na nidhamu hii kunakuwezesha kuchagua, na
kuvumilia mambo fulani katika matendo, fikra na tabia zako, kwa ajili ya
kufanikisha lengo. Inaamsha nguvu za ndani katika kupigana na uvivu.
Moja ya tabia na umuhimu wa hii ni kuepukana na
starehe za muda mfupi sana, kwaajili ya starehe kubwa na zenye kudumu hapo
baadaye ambazo zinahitaji utumie juhudi na muda.
Ujuzi huu
ni moja ya kiambato cha mafanikio. Unajitokeza na kujionyesha kwa njia tofauti:
- Uvumilivu
- Uwezo wa kutokata tamaa, licha ya kufeli na kupata matatizo
- Kujidhibiti
- Uwezo wa kupigana na matatizo na majaribu
Maisha huweka changamoto na matatizo katikati ya
njia ya mafanikio, na ili uyavuke na kuyapita, unahitaji kuishi kwa uvumilivu
na ung’ang’anizi, na hili hasa huhitaji Nidhamu binafsi.
Kuwa na nidhamu hii kunapelekea katika kujiamini,
kujikuza na kuongeza nguvu za ndani, na matokeo yake ni furaha na kuridhika.
Kwa upande mwingine, ukikosa nidhamu binafsi kutakupelekea kufeli, kukosa, matatizo
ya afya na uhusiano, na kuwa na chungu ya matatizo.
Nidhamu binafsi ni zana muhimu sana katika
kurekebisha tabia mbaya na usizopenda kama vile kula sana bila mpangilio,
kuvuta sigara, kulewa na tabia nyinginezo. Unahitaji ukae chini ujifunze na
kuchukua mazoezi kwa kuboresha ujuzi wa aina yoyote ile.
Kama nilivyoeleza hapo mwanzo, ujuzi wa nidhamu
binafsi hufahamika na kuchukuliwa mazoezi na watu wachache sana, wengi hawajui
jinsi ya kuboresha hili. Hii inaboreshwa kwa kuchukua mazoezi kama unavyochukua
mazoezi katika kuboresha ujuzi mwingine.
Nidhamu binafsi au dhana ya
kujiheshimu inakusaidia:
1. Kuepuka kuishi na tabia za hovyo
2. Kutekeleza ahadi zako binafsi na
za wengine
3. Kupigana na uvivu na ukawiaji
4. Kukupa uvumilivu wa kuendelea
kufanya jambo hata kama umefeli
5. Kwenda kufanya mazoezi ya viungo,
hali ya kuwa mwili unatamani kukaa tu na kuangalia TV
6. Kufuata ratiba zako ipasavyo
7. Kuamka asubuhi mapema.
8. Kuondoa tabia ya kuangalia TV
muda mrefu
9. Kujitahidi kufanya mambo ya
muhimu kwa mpangilio mzuri
Itakuwa rahisi kwako kuboresha nguvu ya nidhamu
hii, kama:
- Ukifikiri na kujua umuhimu wake
- Ukijua tabia zako zisizopendeza hata kwako binafsi. Pale unapozidi kuzifahamu tabia hizi, ndipo unapozidi kutafuta njia za kurekebisha
- Ukitengeneza listi ya mambo unayotaka kufanikisha. Hii itatia nguvu motisha.
- Ukifanya juhudi za kuishi vile unavyotaka, mbali na uvivu, hisia za kutaka kuchelewesha jambo au ile tabia ya kukata tamaa na kuacha kile unachofanya.
Hili linaweza kufanikishwa
kabisa hata kama ujuzi wako wa nidhamu hii bado ni mdogo.
“Fanya
kitu sahihi, wakati sahihi na mahali sahihi” Shauri
Mara nyingi tumekuwa tukifahamu nidhamu kwa kuzingatia sana
masuala ya nje kama vile utii, heshima,unyenyekevu na mengine mengi yafananayo
na hayo na kwamba kuwapo na dharau, kiburi, ufanywaji wa mambo ya aibu, unyama
na mengine ni matokeo ya ukosefu wa nidhamu ya ndani ya mtu binafsi (mental
discipline). Lakini hapa tutazungumzia masuala ya nidhamu katika Nyanja zote za
maisha yaani nidhamu binafsi, kimasomo,kikazi, katika mambo ya Mungu,
kifamilia, muda n.k. Nidhamu ya ndani ya mtu ndio inayoweza kufanya mabadiliko
katika ufanisi wa kazi au utendaji wa mambo ya mtu na kubadilisha mfumo mzima
wa Maisha.
Nidhamu ni neno dogo sana kulitamka ila ni kitu kikuu mno
kumfanya mtu kufikia malengo yake na kuwa mtu wa tofauti na watu wengine
wamzungukao. Kinachotofautisha mtu huyu na Yule ni nidhamu yao katika kuishi
kwao.
Maana ya neno nidhamu.
Nidhamu ni ile hali ya mtu kuwa makini katika kufuata
uongozi sahihi au kanuni sahihi ili kufikia malengo yaliyotarajiwa. Na nidhamu
ya ndani ni ile nguvu ya ndani ya mtu ambayo imejengeka, imeimarika kiasi cha
kufanya mambo katika ufanisi na ujuzi wa hali ya juu yaani kufanya kitu sahihi,
wakati sahihi na mahali sahihi ili kufikia kusudi sahihi.
Ni wazi ya kwamba watu tumekuwa tukitafuta matokeo mazuri kiafya, kimasomo, kikazi, kifamilia, kibiashara, kijamii yaani kimaisha kwa ujumla lakini imekuwa ni kazi nzito, ngumu na inayochosha
kufikia malengo hayo, Jiulize je, ninafuata kanuni sahihi na
kwa umakini? kwani mipango tu na juhudi nyingi hazitoshi kuleta matokeo mazuri.
Kunahitajika kitu cha muhimu kinachofuatwa mara kwa mara ili kurahisisha ufikiaji
wa lengo hilo, kitu hicho ni nidhamu.
Pia nidhamu tunaweza kulinganisha na egemeo katika kurahisisha utendaji wa kazi yaani katika nyenzo. Tujikumbushe fizikia
Nyenzo ni kitu ambacho kinatumika katika kurahisisha kazi. Nyenzo ina sehemu kuu tatu yaani mzigo, egemeo na jitihada. Mzigo pekee pamoja na jitihada haviwezi kurahisisha kazi, na muda mwingine kazi huonekana ni ngumu sana kwa kukosekana kwake kwani lazima kuwepo na kitu cha muhimu sana ambacho ni egemeo.
Vivyo hivyo ili kurahisisha utendaji kazi, au ufikiwaji wa malengo husika ya mtu, lazima kuwe na vitu vikuu vitatu vinavvyo ambatana, ambavyo ni malengo, nidhamu pamoja na juhudi. Kuwa na mipango tu, au maono tu pamoja na juhudi nyingi haviwezi kurahisisha kufikia mafanikio yako, lazima kuwe na kitu kimoja cha muhimu kinachotegemewa kurahisisha kazi ambacho ni nidhamu.
Hebu tuangalie kwa upana kidogo kuhusu vipengele mbalimbali
vya ukosefu wa nidhamu
1. Ukosefu wa nidhamu katika muda
Huyu kwa kweli ndiye adui mkubwa ambaye anazuia mafanikio
makubwa ya watu wengi, kwani ana uwezo wa kupoteza, kuharibu na hata kufanya
mipango ya mtu isitimie, kama tulivyomtazama kwa undani wake katika sura
zilizotangulia.
Kusipokuwa na umakini katika kutumia muda, yaani kuwa mahali sahihi, ukifanya kitu sahihi kwa wakati sahihi lazima kunakuwa na upungufu katika kupata matokeo yaliyokusudiwa. Kama maandiko matakatifu yanavyo sema katika kitabu cha Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.”
Kwa hiyo tangu mbingu na nchi ziumbwe, mwanadamu aliumbwa ili afanye mambo yake yote kwa kufuata utaratibu. Mtume Paulo aliwaonya waefeso kuhusu kuutunza muda , alisema “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; Mkiukomboa wakati kwa maana nyakati hizi ni za uovu” Waefeso 5:15-16
Na pia kuna usemi wa kiingereza usemao “you can choose to be the manager of time or the servant of time” it is your choice, ikimaanisha ya kwamba ni wewe tu mwenye maamuzi ya kutumia muda kwa kuuongoza (ukawa meneja) au ukaongozwa na muda (ukawa mtumwa). Hivyo ni vema kupata moyo wa hekima katika kuyafanyia kazi mafundisho haya nawe utakuwa mwenye hekima. Weka nidhamu ya hali ya juu katika kutumia muda wako.
2. Ukosefu wa nidhamu katika mambo ya Mungu
Mungu wetu ni Mungu ambaye yuko makini na anayefuata
utaratibu katika kufanya mambo yake yote. Katika siku sita za uumbaji aliumba
kwa mpangilio thabiti na ndio matokeo mpaka sasa vitu vilivyoumbwa vipo. Vivyo
hivyo kama wana wa Mungu aliye hai imetupasa kutii na kufuata maagizo
anayotuagiza kila siku ili tuwe kama alivyotukusudia.
Wakristo wengi wamekuwa ni watu ambao wanapenda matokeo
mazuri tu katika uhusiano wao na Mungu na kufikiri kwamba unakuja kiurahisi
rahisi. Lahasha! Kuna juhudi zinatakiwa ikiwa na kufuata uongozi kwa ufasaha
ndipo matokeo yanakuja. katika kila
jambo linahitaji kufuata uongozi wa neno la Mungu ambayo ndiyo nidhamu. Ni
kweli yote yanawezekana kwa Mungu tukiamini na zaidi tukiwa na nidhamu kwa
mambo yake.
3. Ukosefu wa nidhamu katika kula/kunywa.
Unaweza dharau na kuona ni jambo dogo sana kutazama masuala
ya afya ila hili ni jambo kubwa sana kwa kuwa mafanikio yako yanategemea sana
afya yako ilivyo, kama afya yako si njema si rahisi kufikia malengo uliyonayo.
Tatizo si chakula ila tatizo ni wewe umekosa nidhamu katika
matumizi ya chakula, kama una nidhamu nzuri utajua ni nini ukile kwa wakati
fulani na nini usile kwa wakati fulani, ukifahamu kuwa kitu fulani kinaweza
kuleta hatari ya afya yako nidhamu inakufundisha uache ili kuitunza afya yako
iwe njema kukusaidia kutimiza malengo uliyonayo katika maisha yako. Mfano kuna
watu wanavuta sigara na kunywa pombe wakifahamu kuwa ni hatari kwa afya zao na
jamii iwazungukayo, jawabu rahisi kutoka kwao ni wamekosa nidhamu ambayo
ingewasaidia kukwepa kwa kuwa nidhamu yatufunza kuwa makini kufanya mambo ya
faida kwetu wenyewe.
Nidhamu katika mfumo mzima wa afya ni wa muhimu sana katika
kuyafikia malengo au ndoto zako. Mungu wetu mwenyewe anataka tuwe na afya njema
wakati wote ndio maana kwa kupigwa kwake
msalabani sisi tumepona yaani tu wazima.
Ili tuweze kuwa na afya njema inatakiwa tujali afya za miili
yetu kwa kutumia chakula bora pamoja na maji safi na salama.
Hapa nitatilia mkazo sana katika suala la kunywa maji, kwani
mwili wetu umejengwa kwa asilimia 100 ambapo 60% ni maji na 40% ni chakula,
kumaanisha ya kwamba 3/5 ya mwili ni maji tu na 2/5 ni chakula. Kwa hiyo inatakiwa tunywe maji kwa
wingi na kwa kufuata utaratibu ili tuikinge miili yetu dhidi ya magonjwa, cha
kushangaza watu wengi wanatumia chakula kwa wingi na maji yanatumiwa kama ya
ziada tu, na zaidi utafiti unaonyesha ya kwamba 90% ya magonjwa yote huanzia
kwenye mfumo wa mmeng’enyo wa chakula hivyo ni wazi kwamba kutozingatia kanuni
sahihi za utumiaji wa lishe bora unapelekea kuibuka kwa magonjwa mengi.
Kwa kawaida kila mtu anapaswa kunywa
maji yasiyopungua lita 3 kwa siku, lakini swali ni hili; je? Unakunywa kiwango
sahihi, wakati sahihi, mahali sahihi ili uweze kupata matokeo sahihi? au
matokeo yoyote? Unaweza ukasema huyu mwandishi anaongea nini, jibu ni kwamba
kama unataka upate matokeo sahihi ni lazima ufuate kanuni sahihi. Hapa
nitakufundisha kanuni rahisi sana itakayokusaidia kunywa maji na kupata matokeo
mazuri maana imefanyiwa utafiti, kujaribiwa na hata kutumiwa kwa miaka mingi na
matokeo tunayaona.
Kwanza unapoamka alfajiri kwa ajili ya maombi, mazoezi au
kujiandaa ni lazima unywe 150cl ambayo ni sawa na lita 1.5 kwa muda wa dakika 2
̶ 5. Na muda unaofaa ni (saa 10, 11 na 12) alfajiri kulingana na muda
unaoamka ukichelewa sana saa 1 asubuhi. Imethibitishwa kwamba maji yanayonywewa
muda huu yana umuhimu mkubwa sana katika ufanisi wa kazi zako za siku nzima.
Pili mchana saa moja kabla, au baada ya chakula kati ya
saa7, 8 hadi 9 unakunywa 75cl ambazo ni sawa na 3/4 ya lita. Vivyo hivyo na jioni kati saa (12,1
na 2 )usiku unakunywa robo tatu ya lita
yaani 1/2 +1/4. Maji yanayoshauriwa kutumiwa ni ya kawaida
usipende kutumia maji ya baridi.
Ukianza kuifuata kanuni hii itakusaidia kufanya kazi kwa ufanisi, kwa muda mrefu na kuufanya ubongo wako ufanye kazi vizuri, pia itakukinga dhidi ya maradhi kwani kila sehemu ya mwili imepata kiasi chake cha maji kinachotakiwa. Sio hivyo tu bali utalala kwa wakati unaostahili kulala na utaamka kwa muda unaopaswa hivyo kuzuia kusinzia wakati wa kazi/ibaada/mikutano n.k. Kwa wiki mbili za kwanza unapoanza unaweza ukaona ni kazi sana kwani unakunywa maji kwa muda usio na kiu bali kuanzia wiki ya tatu itakuwa ni tabia yako iliyojengeka na kuimarika na utayafurahia matokeo yake.
Pia kuhusu umuhimu wa maji katika Maisha ya mtu, naomba
utafakari sana kuhusu UUMBAJI katika
kitabu cha Mwanzo 1:2 “Nayo nchi ilikuwa
ukiwa,tena utupu,na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu
ikatulia juu ya uso wa maji” Hivi? Kwanini roho wa Mungu alikaa juu ya maji
na sio chini kwenye vilindi au mbinguni? Hii ni kuonyesha kwamba alikuwa
anaatamia uumbaji (kuumbwa kwa nchi) hivyo hata kama hali uliyonayo ni ya ukiwa
kiasi gani, maji ni ya muhimu sana katika kuumba afya njema.
Kwa kuwa afya njema ni ya muhimu sana kwa mafanikio ya mtu,
Big Results Now (BRN) yaani matokeo makubwa sasa kwa afya yako yanawezekana kwa
kufuata utaratibu sahihi ulioelekezwa. Wewe andaa maji yako tu, na uyatumie.
Daudi
anamuomba Mungu na kumwambia “Basi
utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima” na katika
tafsiri ya The Living Bible usema “Teach
us to number our days. And recognize how few they are, help us to spend them as
we should,” utafsiri maneno haya kwa Kiswahili chake kuwa “Utufundishe kuhesabu siku zetu. Tujue ni jinsi zilivyo chache,
utusaidie kuzitumia jinsi itupasavyo.” Zaburi 90.12. Daudi kwa kuwa na
hekima alifahamu kuna umuhimu sana wa kujua siku zake kuwa zi chache na kuna
umuhimu mkubwa sana wa kuishi kwa hekima katika siku hizo. Ni dhahiri kuwa kama
hujui kuwa una siku chache za kuishi duniani ni kazi kwako kuishi kwa hekima na
hata kujua ni namna gani unapaswa kufanya hili afya yako iwe chache sana.
- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2015/05/somo-kukosa-nidhamu-ya-maisha-ni.html#sthash.pw7O4UEe.dpuf
“Fanya
kitu sahihi, wakati sahihi na mahali sahihi” Shauri
Mara nyingi tumekuwa tukifahamu nidhamu kwa kuzingatia sana
masuala ya nje kama vile utii, heshima,unyenyekevu na mengine mengi yafananayo
na hayo na kwamba kuwapo na dharau, kiburi, ufanywaji wa mambo ya aibu, unyama
na mengine ni matokeo ya ukosefu wa nidhamu ya ndani ya mtu binafsi (mental
discipline). Lakini hapa tutazungumzia masuala ya nidhamu katika Nyanja zote za
maisha yaani nidhamu binafsi, kimasomo,kikazi, katika mambo ya Mungu,
kifamilia, muda n.k. Nidhamu ya ndani ya mtu ndio inayoweza kufanya mabadiliko
katika ufanisi wa kazi au utendaji wa mambo ya mtu na kubadilisha mfumo mzima
wa Maisha.
Nidhamu ni neno dogo sana kulitamka ila ni kitu kikuu mno
kumfanya mtu kufikia malengo yake na kuwa mtu wa tofauti na watu wengine
wamzungukao. Kinachotofautisha mtu huyu na Yule ni nidhamu yao katika kuishi
kwao.
Maana ya neno nidhamu.
Nidhamu ni ile hali ya mtu kuwa makini katika kufuata
uongozi sahihi au kanuni sahihi ili kufikia malengo yaliyotarajiwa. Na nidhamu
ya ndani ni ile nguvu ya ndani ya mtu ambayo imejengeka, imeimarika kiasi cha
kufanya mambo katika ufanisi na ujuzi wa hali ya juu yaani kufanya kitu sahihi,
wakati sahihi na mahali sahihi ili kufikia kusudi sahihi.
Ni wazi ya kwamba watu tumekuwa tukitafuta matokeo mazuri kiafya, kimasomo, kikazi, kifamilia, kibiashara, kijamii yaani kimaisha kwa ujumla lakini imekuwa ni kazi nzito, ngumu na inayochosha
kufikia malengo hayo, Jiulize je, ninafuata kanuni sahihi na
kwa umakini? kwani mipango tu na juhudi nyingi hazitoshi kuleta matokeo mazuri.
Kunahitajika kitu cha muhimu kinachofuatwa mara kwa mara ili kurahisisha ufikiaji
wa lengo hilo, kitu hicho ni nidhamu.
Pia nidhamu tunaweza kulinganisha na egemeo katika kurahisisha utendaji wa kazi yaani katika nyenzo. Tujikumbushe fizikia
Nyenzo ni kitu ambacho kinatumika katika kurahisisha kazi. Nyenzo ina sehemu kuu tatu yaani mzigo, egemeo na jitihada. Mzigo pekee pamoja na jitihada haviwezi kurahisisha kazi, na muda mwingine kazi huonekana ni ngumu sana kwa kukosekana kwake kwani lazima kuwepo na kitu cha muhimu sana ambacho ni egemeo.
Vivyo hivyo ili kurahisisha utendaji kazi, au ufikiwaji wa malengo husika ya mtu, lazima kuwe na vitu vikuu vitatu vinavvyo ambatana, ambavyo ni malengo, nidhamu pamoja na juhudi. Kuwa na mipango tu, au maono tu pamoja na juhudi nyingi haviwezi kurahisisha kufikia mafanikio yako, lazima kuwe na kitu kimoja cha muhimu kinachotegemewa kurahisisha kazi ambacho ni nidhamu.
Hebu tuangalie kwa upana kidogo kuhusu vipengele mbalimbali
vya ukosefu wa nidhamu
1. Ukosefu wa nidhamu katika muda
Huyu kwa kweli ndiye adui mkubwa ambaye anazuia mafanikio
makubwa ya watu wengi, kwani ana uwezo wa kupoteza, kuharibu na hata kufanya
mipango ya mtu isitimie, kama tulivyomtazama kwa undani wake katika sura
zilizotangulia.
Kusipokuwa na umakini katika kutumia muda, yaani kuwa mahali sahihi, ukifanya kitu sahihi kwa wakati sahihi lazima kunakuwa na upungufu katika kupata matokeo yaliyokusudiwa. Kama maandiko matakatifu yanavyo sema katika kitabu cha Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.”
Kwa hiyo tangu mbingu na nchi ziumbwe, mwanadamu aliumbwa ili afanye mambo yake yote kwa kufuata utaratibu. Mtume Paulo aliwaonya waefeso kuhusu kuutunza muda , alisema “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; Mkiukomboa wakati kwa maana nyakati hizi ni za uovu” Waefeso 5:15-16
Na pia kuna usemi wa kiingereza usemao “you can choose to be the manager of time or the servant of time” it is your choice, ikimaanisha ya kwamba ni wewe tu mwenye maamuzi ya kutumia muda kwa kuuongoza (ukawa meneja) au ukaongozwa na muda (ukawa mtumwa). Hivyo ni vema kupata moyo wa hekima katika kuyafanyia kazi mafundisho haya nawe utakuwa mwenye hekima. Weka nidhamu ya hali ya juu katika kutumia muda wako.
2. Ukosefu wa nidhamu katika mambo ya Mungu
Mungu wetu ni Mungu ambaye yuko makini na anayefuata
utaratibu katika kufanya mambo yake yote. Katika siku sita za uumbaji aliumba
kwa mpangilio thabiti na ndio matokeo mpaka sasa vitu vilivyoumbwa vipo. Vivyo
hivyo kama wana wa Mungu aliye hai imetupasa kutii na kufuata maagizo
anayotuagiza kila siku ili tuwe kama alivyotukusudia.
Wakristo wengi wamekuwa ni watu ambao wanapenda matokeo
mazuri tu katika uhusiano wao na Mungu na kufikiri kwamba unakuja kiurahisi
rahisi. Lahasha! Kuna juhudi zinatakiwa ikiwa na kufuata uongozi kwa ufasaha
ndipo matokeo yanakuja. katika kila
jambo linahitaji kufuata uongozi wa neno la Mungu ambayo ndiyo nidhamu. Ni
kweli yote yanawezekana kwa Mungu tukiamini na zaidi tukiwa na nidhamu kwa
mambo yake.
3. Ukosefu wa nidhamu katika kula/kunywa.
Unaweza dharau na kuona ni jambo dogo sana kutazama masuala
ya afya ila hili ni jambo kubwa sana kwa kuwa mafanikio yako yanategemea sana
afya yako ilivyo, kama afya yako si njema si rahisi kufikia malengo uliyonayo.
Tatizo si chakula ila tatizo ni wewe umekosa nidhamu katika
matumizi ya chakula, kama una nidhamu nzuri utajua ni nini ukile kwa wakati
fulani na nini usile kwa wakati fulani, ukifahamu kuwa kitu fulani kinaweza
kuleta hatari ya afya yako nidhamu inakufundisha uache ili kuitunza afya yako
iwe njema kukusaidia kutimiza malengo uliyonayo katika maisha yako. Mfano kuna
watu wanavuta sigara na kunywa pombe wakifahamu kuwa ni hatari kwa afya zao na
jamii iwazungukayo, jawabu rahisi kutoka kwao ni wamekosa nidhamu ambayo
ingewasaidia kukwepa kwa kuwa nidhamu yatufunza kuwa makini kufanya mambo ya
faida kwetu wenyewe.
Nidhamu katika mfumo mzima wa afya ni wa muhimu sana katika
kuyafikia malengo au ndoto zako. Mungu wetu mwenyewe anataka tuwe na afya njema
wakati wote ndio maana kwa kupigwa kwake
msalabani sisi tumepona yaani tu wazima.
Ili tuweze kuwa na afya njema inatakiwa tujali afya za miili
yetu kwa kutumia chakula bora pamoja na maji safi na salama.
Hapa nitatilia mkazo sana katika suala la kunywa maji, kwani
mwili wetu umejengwa kwa asilimia 100 ambapo 60% ni maji na 40% ni chakula,
kumaanisha ya kwamba 3/5 ya mwili ni maji tu na 2/5 ni chakula. Kwa hiyo inatakiwa tunywe maji kwa
wingi na kwa kufuata utaratibu ili tuikinge miili yetu dhidi ya magonjwa, cha
kushangaza watu wengi wanatumia chakula kwa wingi na maji yanatumiwa kama ya
ziada tu, na zaidi utafiti unaonyesha ya kwamba 90% ya magonjwa yote huanzia
kwenye mfumo wa mmeng’enyo wa chakula hivyo ni wazi kwamba kutozingatia kanuni
sahihi za utumiaji wa lishe bora unapelekea kuibuka kwa magonjwa mengi.
Kwa kawaida kila mtu anapaswa kunywa
maji yasiyopungua lita 3 kwa siku, lakini swali ni hili; je? Unakunywa kiwango
sahihi, wakati sahihi, mahali sahihi ili uweze kupata matokeo sahihi? au
matokeo yoyote? Unaweza ukasema huyu mwandishi anaongea nini, jibu ni kwamba
kama unataka upate matokeo sahihi ni lazima ufuate kanuni sahihi. Hapa
nitakufundisha kanuni rahisi sana itakayokusaidia kunywa maji na kupata matokeo
mazuri maana imefanyiwa utafiti, kujaribiwa na hata kutumiwa kwa miaka mingi na
matokeo tunayaona.
Kwanza unapoamka alfajiri kwa ajili ya maombi, mazoezi au
kujiandaa ni lazima unywe 150cl ambayo ni sawa na lita 1.5 kwa muda wa dakika 2
̶ 5. Na muda unaofaa ni (saa 10, 11 na 12) alfajiri kulingana na muda
unaoamka ukichelewa sana saa 1 asubuhi. Imethibitishwa kwamba maji yanayonywewa
muda huu yana umuhimu mkubwa sana katika ufanisi wa kazi zako za siku nzima.
Pili mchana saa moja kabla, au baada ya chakula kati ya
saa7, 8 hadi 9 unakunywa 75cl ambazo ni sawa na 3/4 ya lita. Vivyo hivyo na jioni kati saa (12,1
na 2 )usiku unakunywa robo tatu ya lita
yaani 1/2 +1/4. Maji yanayoshauriwa kutumiwa ni ya kawaida
usipende kutumia maji ya baridi.
Ukianza kuifuata kanuni hii itakusaidia kufanya kazi kwa ufanisi, kwa muda mrefu na kuufanya ubongo wako ufanye kazi vizuri, pia itakukinga dhidi ya maradhi kwani kila sehemu ya mwili imepata kiasi chake cha maji kinachotakiwa. Sio hivyo tu bali utalala kwa wakati unaostahili kulala na utaamka kwa muda unaopaswa hivyo kuzuia kusinzia wakati wa kazi/ibaada/mikutano n.k. Kwa wiki mbili za kwanza unapoanza unaweza ukaona ni kazi sana kwani unakunywa maji kwa muda usio na kiu bali kuanzia wiki ya tatu itakuwa ni tabia yako iliyojengeka na kuimarika na utayafurahia matokeo yake.
Pia kuhusu umuhimu wa maji katika Maisha ya mtu, naomba
utafakari sana kuhusu UUMBAJI katika
kitabu cha Mwanzo 1:2 “Nayo nchi ilikuwa
ukiwa,tena utupu,na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu
ikatulia juu ya uso wa maji” Hivi? Kwanini roho wa Mungu alikaa juu ya maji
na sio chini kwenye vilindi au mbinguni? Hii ni kuonyesha kwamba alikuwa
anaatamia uumbaji (kuumbwa kwa nchi) hivyo hata kama hali uliyonayo ni ya ukiwa
kiasi gani, maji ni ya muhimu sana katika kuumba afya njema.
Kwa kuwa afya njema ni ya muhimu sana kwa mafanikio ya mtu,
Big Results Now (BRN) yaani matokeo makubwa sasa kwa afya yako yanawezekana kwa
kufuata utaratibu sahihi ulioelekezwa. Wewe andaa maji yako tu, na uyatumie.
Daudi
anamuomba Mungu na kumwambia “Basi
utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima” na katika
tafsiri ya The Living Bible usema “Teach
us to number our days. And recognize how few they are, help us to spend them as
we should,” utafsiri maneno haya kwa Kiswahili chake kuwa “Utufundishe kuhesabu siku zetu. Tujue ni jinsi zilivyo chache,
utusaidie kuzitumia jinsi itupasavyo.” Zaburi 90.12. Daudi kwa kuwa na
hekima alifahamu kuna umuhimu sana wa kujua siku zake kuwa zi chache na kuna
umuhimu mkubwa sana wa kuishi kwa hekima katika siku hizo. Ni dhahiri kuwa kama
hujui kuwa una siku chache za kuishi duniani ni kazi kwako kuishi kwa hekima na
hata kujua ni namna gani unapaswa kufanya hili afya yako iwe chache sana.
- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2015/05/somo-kukosa-nidhamu-ya-maisha-ni.html#sthash.pw7O4UEe.dpuf
No comments:
Post a Comment