Wednesday 20 April 2016

Faida na umuhimu wa dhana ya kujiheshimu



Tumeona jinsi ya kuchukua mazoezi ya kuboresha dhana ya kujiheshimu au nidhamu binafsi katika makala iliyopita.
Kwa kukukumbusha:
Nidhamu binafsi au dhana ya kujiheshimu ni ile hali ya kufanya kile kizuri unachopaswa kukifanya kwa kujilazimisha kukifanya ukijitahidi kupingana na uvivu na mambo yanayokusababisha usikifanye.
Moja ya ujuzi wenye umuhimu na thamani kubwa sana ambao kila mtu anapaswa awe nao ni nidhamu binafsi. Ni ujuzi ambao unahitajika katika kila kona ya maisha yako. Wengi hawajui umuhimu wa hii na ndio maana wachache sana hufanyia kazi kutia nguvu nidhamu hii.
Kinyume cha imani ya kawaida, nidhamu binafsi siyo tabia ya kujibana, kujinyima uhuru fulani. Inaongeza chembechembe za kujidhibiti, akili na uvumilivu katika maisha yako. Hii ina maana kuwa itakufanya uwe na uwezo mkubwa wa udhibiti wa mambo kadha katika maisha yako.
Nidhamu binafsi inakupa nguvu za kudumu katika uamuzi wako na kuufuata, bil akubadilisha uamuzi wako na kuyumbayumba, na hivyo hii ni moja ya zana muhimu sana katika ufanikishaji wa malengo.
Kuwa na nidhamu hii kunakuwezesha kuchagua, na kuvumilia mambo fulani katika matendo, fikra na tabia zako, kwa ajili ya kufanikisha lengo. Inaamsha nguvu za ndani katika kupigana na uvivu.
Moja ya tabia na umuhimu wa hii ni kuepukana na starehe za muda mfupi sana, kwaajili ya starehe kubwa na zenye kudumu hapo baadaye ambazo zinahitaji utumie juhudi na muda.
Ujuzi huu ni moja ya kiambato cha mafanikio. Unajitokeza na kujionyesha kwa njia tofauti:

  1. Uvumilivu
  2. Uwezo wa kutokata tamaa, licha ya kufeli na kupata matatizo
  3. Kujidhibiti
  4. Uwezo wa kupigana na matatizo na majaribu
Maisha huweka changamoto na matatizo katikati ya njia ya mafanikio, na ili uyavuke na kuyapita, unahitaji kuishi kwa uvumilivu na ung’ang’anizi, na hili hasa huhitaji Nidhamu binafsi.
Kuwa na nidhamu hii kunapelekea katika kujiamini, kujikuza na kuongeza nguvu za ndani, na matokeo yake ni furaha na kuridhika. Kwa upande mwingine, ukikosa nidhamu binafsi kutakupelekea kufeli, kukosa, matatizo ya afya na uhusiano, na kuwa na chungu ya matatizo.
Nidhamu binafsi ni zana muhimu sana katika kurekebisha tabia mbaya na usizopenda kama vile kula sana bila mpangilio, kuvuta sigara, kulewa na tabia nyinginezo. Unahitaji ukae chini ujifunze na kuchukua mazoezi kwa kuboresha ujuzi wa aina yoyote ile.
Kama nilivyoeleza hapo mwanzo, ujuzi wa nidhamu binafsi hufahamika na kuchukuliwa mazoezi na watu wachache sana, wengi hawajui jinsi ya kuboresha hili. Hii inaboreshwa kwa kuchukua mazoezi kama unavyochukua mazoezi katika kuboresha ujuzi mwingine.
Nidhamu binafsi au dhana ya kujiheshimu inakusaidia:
1.      Kuepuka kuishi na tabia za hovyo
2.      Kutekeleza ahadi zako binafsi na za wengine
3.      Kupigana na uvivu na ukawiaji
4.      Kukupa uvumilivu wa kuendelea kufanya jambo hata kama umefeli
5.      Kwenda kufanya mazoezi ya viungo, hali ya kuwa mwili unatamani kukaa tu na kuangalia TV
6.      Kufuata ratiba zako ipasavyo
7.      Kuamka asubuhi mapema.
8.      Kuondoa tabia ya kuangalia TV muda mrefu
9.      Kujitahidi kufanya mambo ya muhimu kwa mpangilio mzuri
Itakuwa rahisi kwako kuboresha nguvu ya nidhamu hii, kama:
  1. Ukifikiri na kujua umuhimu wake
  2. Ukijua tabia zako zisizopendeza hata kwako binafsi. Pale unapozidi kuzifahamu tabia hizi, ndipo unapozidi kutafuta njia za kurekebisha
  3. Ukitengeneza listi ya mambo unayotaka kufanikisha. Hii itatia nguvu motisha.
  4. Ukifanya juhudi za kuishi vile unavyotaka, mbali na uvivu, hisia za kutaka kuchelewesha jambo au ile tabia ya kukata tamaa na kuacha kile unachofanya.
Hili linaweza kufanikishwa kabisa hata kama ujuzi wako wa nidhamu hii bado ni mdogo.
“Fanya kitu sahihi, wakati sahihi na mahali sahihi” Shauri
Mara nyingi tumekuwa tukifahamu nidhamu kwa kuzingatia sana masuala ya nje kama vile utii, heshima,unyenyekevu na mengine mengi yafananayo na hayo na kwamba kuwapo na dharau, kiburi, ufanywaji wa mambo ya aibu, unyama na mengine ni matokeo ya ukosefu wa nidhamu ya ndani ya mtu binafsi (mental discipline). Lakini hapa tutazungumzia masuala ya nidhamu katika Nyanja zote za maisha yaani nidhamu binafsi, kimasomo,kikazi, katika mambo ya Mungu, kifamilia, muda n.k. Nidhamu ya ndani ya mtu ndio inayoweza kufanya mabadiliko katika ufanisi wa kazi au utendaji wa mambo ya mtu na kubadilisha mfumo mzima wa Maisha.
Nidhamu ni neno dogo sana kulitamka ila ni kitu kikuu mno kumfanya mtu kufikia malengo yake na kuwa mtu wa tofauti na watu wengine wamzungukao. Kinachotofautisha mtu huyu na Yule ni nidhamu yao katika kuishi kwao.

Maana ya neno nidhamu.
Nidhamu ni ile hali ya mtu kuwa makini katika kufuata uongozi sahihi au kanuni sahihi ili kufikia malengo yaliyotarajiwa. Na nidhamu ya ndani ni ile nguvu ya ndani ya mtu ambayo imejengeka, imeimarika kiasi cha kufanya mambo katika ufanisi na ujuzi wa hali ya juu yaani kufanya kitu sahihi, wakati sahihi na mahali sahihi ili kufikia kusudi sahihi.

Ni wazi ya kwamba watu tumekuwa tukitafuta matokeo mazuri kiafya, kimasomo, kikazi, kifamilia, kibiashara, kijamii yaani kimaisha kwa ujumla lakini imekuwa ni kazi nzito, ngumu na inayochosha


kufikia malengo hayo, Jiulize je, ninafuata kanuni sahihi na kwa umakini? kwani mipango tu na juhudi nyingi hazitoshi kuleta matokeo mazuri. Kunahitajika kitu cha muhimu kinachofuatwa mara kwa mara ili kurahisisha ufikiaji wa lengo hilo, kitu hicho ni nidhamu.

Pia nidhamu tunaweza kulinganisha na egemeo katika kurahisisha utendaji wa kazi yaani katika nyenzo.  Tujikumbushe fizikia

Nyenzo ni kitu ambacho kinatumika katika kurahisisha kazi. Nyenzo ina sehemu kuu tatu yaani mzigo, egemeo na jitihada.  Mzigo pekee pamoja na jitihada haviwezi kurahisisha kazi, na muda mwingine kazi huonekana ni ngumu sana kwa kukosekana kwake kwani lazima kuwepo na kitu cha muhimu sana ambacho ni egemeo.

Vivyo hivyo ili kurahisisha utendaji kazi, au ufikiwaji wa malengo husika ya mtu, lazima kuwe na vitu vikuu vitatu vinavvyo ambatana, ambavyo ni malengo, nidhamu pamoja na juhudi. Kuwa na mipango tu, au maono tu  pamoja na juhudi nyingi haviwezi kurahisisha kufikia mafanikio yako, lazima kuwe na kitu kimoja cha muhimu kinachotegemewa kurahisisha kazi ambacho ni nidhamu.
Hebu tuangalie kwa upana kidogo kuhusu vipengele mbalimbali vya ukosefu wa nidhamu

1.    Ukosefu wa nidhamu katika muda
Huyu kwa kweli ndiye adui mkubwa ambaye anazuia mafanikio makubwa ya watu wengi, kwani ana uwezo wa kupoteza, kuharibu na hata kufanya mipango ya mtu isitimie, kama tulivyomtazama kwa undani wake katika sura zilizotangulia.

Kusipokuwa na umakini katika kutumia muda, yaani kuwa mahali sahihi, ukifanya kitu sahihi kwa wakati sahihi lazima kunakuwa na upungufu katika kupata matokeo yaliyokusudiwa. Kama maandiko matakatifu yanavyo sema katika kitabu cha Mhubiri 3:1Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.”

Kwa hiyo tangu mbingu na nchi ziumbwe, mwanadamu aliumbwa ili afanye mambo yake yote kwa kufuata utaratibu. Mtume Paulo aliwaonya waefeso kuhusu kuutunza muda , alisema  “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; Mkiukomboa wakati kwa maana nyakati hizi ni za uovu” Waefeso 5:15-16

Na pia kuna usemi wa kiingereza usemao “you can choose to be the manager of time or the servant of time” it is your choice, ikimaanisha ya kwamba ni wewe tu mwenye maamuzi ya kutumia muda kwa kuuongoza (ukawa meneja) au ukaongozwa na muda (ukawa mtumwa). Hivyo ni vema kupata moyo wa hekima katika kuyafanyia kazi mafundisho haya nawe utakuwa mwenye hekima. Weka nidhamu ya hali ya juu katika kutumia muda wako.
2.    Ukosefu wa nidhamu katika mambo ya Mungu
Mungu wetu ni Mungu ambaye yuko makini na anayefuata utaratibu katika kufanya mambo yake yote. Katika siku sita za uumbaji aliumba kwa mpangilio thabiti na ndio matokeo mpaka sasa vitu vilivyoumbwa vipo. Vivyo hivyo kama wana wa Mungu aliye hai imetupasa kutii na kufuata maagizo anayotuagiza kila siku ili tuwe kama alivyotukusudia.
Wakristo wengi wamekuwa ni watu ambao wanapenda matokeo mazuri tu katika uhusiano wao na Mungu na kufikiri kwamba unakuja kiurahisi rahisi. Lahasha! Kuna juhudi zinatakiwa ikiwa na kufuata uongozi kwa ufasaha ndipo matokeo yanakuja.   katika kila jambo linahitaji kufuata uongozi wa neno la Mungu ambayo ndiyo nidhamu. Ni kweli yote yanawezekana kwa Mungu tukiamini na zaidi tukiwa na nidhamu kwa mambo yake.
3.    Ukosefu wa nidhamu katika kula/kunywa.
Unaweza dharau na kuona ni jambo dogo sana kutazama masuala ya afya ila hili ni jambo kubwa sana kwa kuwa mafanikio yako yanategemea sana afya yako ilivyo, kama afya yako si njema si rahisi kufikia malengo uliyonayo.
Tatizo si chakula ila tatizo ni wewe umekosa nidhamu katika matumizi ya chakula, kama una nidhamu nzuri utajua ni nini ukile kwa wakati fulani na nini usile kwa wakati fulani, ukifahamu kuwa kitu fulani kinaweza kuleta hatari ya afya yako nidhamu inakufundisha uache ili kuitunza afya yako iwe njema kukusaidia kutimiza malengo uliyonayo katika maisha yako. Mfano kuna watu wanavuta sigara na kunywa pombe wakifahamu kuwa ni hatari kwa afya zao na jamii iwazungukayo, jawabu rahisi kutoka kwao ni wamekosa nidhamu ambayo ingewasaidia kukwepa kwa kuwa nidhamu yatufunza kuwa makini kufanya mambo ya faida kwetu wenyewe.
Nidhamu katika mfumo mzima wa afya ni wa muhimu sana katika kuyafikia malengo au ndoto zako. Mungu wetu mwenyewe anataka tuwe na afya njema wakati wote ndio maana kwa kupigwa kwake msalabani sisi tumepona yaani tu wazima.
Ili tuweze kuwa na afya njema inatakiwa tujali afya za miili yetu kwa kutumia chakula bora pamoja na maji safi na salama.
Hapa nitatilia mkazo sana katika suala la kunywa maji, kwani mwili wetu umejengwa kwa asilimia 100 ambapo 60% ni maji na 40% ni chakula, kumaanisha ya kwamba 3/5 ya mwili ni maji tu na 2/5 ni chakula. Kwa hiyo inatakiwa tunywe maji kwa wingi na kwa kufuata utaratibu ili tuikinge miili yetu dhidi ya magonjwa, cha kushangaza watu wengi wanatumia chakula kwa wingi na maji yanatumiwa kama ya ziada tu, na zaidi utafiti unaonyesha ya kwamba 90% ya magonjwa yote huanzia kwenye mfumo wa mmeng’enyo wa chakula hivyo ni wazi kwamba kutozingatia kanuni sahihi za utumiaji wa lishe bora unapelekea kuibuka kwa magonjwa mengi.
Kwa kawaida kila mtu anapaswa kunywa maji yasiyopungua lita 3 kwa siku, lakini swali ni hili; je? Unakunywa kiwango sahihi, wakati sahihi, mahali sahihi ili uweze kupata matokeo sahihi? au matokeo yoyote? Unaweza ukasema huyu mwandishi anaongea nini, jibu ni kwamba kama unataka upate matokeo sahihi ni lazima ufuate kanuni sahihi. Hapa nitakufundisha kanuni rahisi sana itakayokusaidia kunywa maji na kupata matokeo mazuri maana imefanyiwa utafiti, kujaribiwa na hata kutumiwa kwa miaka mingi na matokeo tunayaona.
Kwanza unapoamka alfajiri kwa ajili ya maombi, mazoezi au kujiandaa ni lazima unywe 150cl ambayo ni sawa na lita 1.5 kwa muda wa dakika 2  ̶ 5. Na muda unaofaa ni (saa 10, 11 na 12) alfajiri kulingana na muda unaoamka ukichelewa sana saa 1 asubuhi. Imethibitishwa kwamba maji yanayonywewa muda huu yana umuhimu mkubwa sana katika ufanisi wa kazi zako za siku nzima.
Pili mchana saa moja kabla, au baada ya chakula kati ya saa7, 8 hadi 9 unakunywa 75cl ambazo ni sawa na 3/4 ya lita. Vivyo hivyo na jioni kati saa (12,1 na  2 )usiku unakunywa robo tatu ya lita yaani 1/2 +1/4.  Maji yanayoshauriwa kutumiwa ni ya kawaida usipende kutumia maji ya baridi. 

Ukianza kuifuata kanuni hii itakusaidia kufanya kazi kwa ufanisi, kwa muda mrefu na kuufanya ubongo wako ufanye kazi vizuri, pia itakukinga dhidi ya maradhi kwani kila sehemu ya mwili imepata kiasi chake cha maji kinachotakiwa. Sio hivyo tu bali utalala kwa wakati unaostahili kulala na utaamka kwa muda unaopaswa hivyo kuzuia kusinzia wakati wa kazi/ibaada/mikutano n.k.  Kwa wiki mbili za kwanza unapoanza unaweza ukaona ni kazi sana kwani unakunywa maji kwa muda usio na kiu bali kuanzia wiki ya tatu itakuwa ni tabia yako iliyojengeka na kuimarika na utayafurahia matokeo yake.
Pia kuhusu umuhimu wa maji katika Maisha ya mtu, naomba utafakari sana kuhusu UUMBAJI katika kitabu cha Mwanzo 1:2 “Nayo nchi ilikuwa ukiwa,tena utupu,na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji” Hivi? Kwanini roho wa Mungu alikaa juu ya maji na sio chini kwenye vilindi au mbinguni? Hii ni kuonyesha kwamba alikuwa anaatamia uumbaji (kuumbwa kwa nchi) hivyo hata kama hali uliyonayo ni ya ukiwa kiasi gani, maji ni ya muhimu sana katika kuumba afya njema.
Kwa kuwa afya njema ni ya muhimu sana kwa mafanikio ya mtu, Big Results Now (BRN) yaani matokeo makubwa sasa kwa afya yako yanawezekana kwa kufuata utaratibu sahihi ulioelekezwa. Wewe andaa maji yako tu, na uyatumie.
Daudi anamuomba Mungu na kumwambia “Basi utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima” na katika tafsiri ya The Living Bible usema “Teach us to number our days. And recognize how few they are, help us to spend them as we should,” utafsiri maneno haya kwa Kiswahili chake kuwa Utufundishe kuhesabu siku zetu. Tujue ni jinsi zilivyo chache, utusaidie kuzitumia jinsi itupasavyo.” Zaburi 90.12. Daudi kwa kuwa na hekima alifahamu kuna umuhimu sana wa kujua siku zake kuwa zi chache na kuna umuhimu mkubwa sana wa kuishi kwa hekima katika siku hizo. Ni dhahiri kuwa kama hujui kuwa una siku chache za kuishi duniani ni kazi kwako kuishi kwa hekima na hata kujua ni namna gani unapaswa kufanya hili afya yako iwe chache sana.
- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2015/05/somo-kukosa-nidhamu-ya-maisha-ni.html#sthash.pw7O4UEe.dpuf
“Fanya kitu sahihi, wakati sahihi na mahali sahihi” Shauri
Mara nyingi tumekuwa tukifahamu nidhamu kwa kuzingatia sana masuala ya nje kama vile utii, heshima,unyenyekevu na mengine mengi yafananayo na hayo na kwamba kuwapo na dharau, kiburi, ufanywaji wa mambo ya aibu, unyama na mengine ni matokeo ya ukosefu wa nidhamu ya ndani ya mtu binafsi (mental discipline). Lakini hapa tutazungumzia masuala ya nidhamu katika Nyanja zote za maisha yaani nidhamu binafsi, kimasomo,kikazi, katika mambo ya Mungu, kifamilia, muda n.k. Nidhamu ya ndani ya mtu ndio inayoweza kufanya mabadiliko katika ufanisi wa kazi au utendaji wa mambo ya mtu na kubadilisha mfumo mzima wa Maisha.
Nidhamu ni neno dogo sana kulitamka ila ni kitu kikuu mno kumfanya mtu kufikia malengo yake na kuwa mtu wa tofauti na watu wengine wamzungukao. Kinachotofautisha mtu huyu na Yule ni nidhamu yao katika kuishi kwao.

Maana ya neno nidhamu.
Nidhamu ni ile hali ya mtu kuwa makini katika kufuata uongozi sahihi au kanuni sahihi ili kufikia malengo yaliyotarajiwa. Na nidhamu ya ndani ni ile nguvu ya ndani ya mtu ambayo imejengeka, imeimarika kiasi cha kufanya mambo katika ufanisi na ujuzi wa hali ya juu yaani kufanya kitu sahihi, wakati sahihi na mahali sahihi ili kufikia kusudi sahihi.

Ni wazi ya kwamba watu tumekuwa tukitafuta matokeo mazuri kiafya, kimasomo, kikazi, kifamilia, kibiashara, kijamii yaani kimaisha kwa ujumla lakini imekuwa ni kazi nzito, ngumu na inayochosha


kufikia malengo hayo, Jiulize je, ninafuata kanuni sahihi na kwa umakini? kwani mipango tu na juhudi nyingi hazitoshi kuleta matokeo mazuri. Kunahitajika kitu cha muhimu kinachofuatwa mara kwa mara ili kurahisisha ufikiaji wa lengo hilo, kitu hicho ni nidhamu.

Pia nidhamu tunaweza kulinganisha na egemeo katika kurahisisha utendaji wa kazi yaani katika nyenzo.  Tujikumbushe fizikia

Nyenzo ni kitu ambacho kinatumika katika kurahisisha kazi. Nyenzo ina sehemu kuu tatu yaani mzigo, egemeo na jitihada.  Mzigo pekee pamoja na jitihada haviwezi kurahisisha kazi, na muda mwingine kazi huonekana ni ngumu sana kwa kukosekana kwake kwani lazima kuwepo na kitu cha muhimu sana ambacho ni egemeo.

Vivyo hivyo ili kurahisisha utendaji kazi, au ufikiwaji wa malengo husika ya mtu, lazima kuwe na vitu vikuu vitatu vinavvyo ambatana, ambavyo ni malengo, nidhamu pamoja na juhudi. Kuwa na mipango tu, au maono tu  pamoja na juhudi nyingi haviwezi kurahisisha kufikia mafanikio yako, lazima kuwe na kitu kimoja cha muhimu kinachotegemewa kurahisisha kazi ambacho ni nidhamu.
Hebu tuangalie kwa upana kidogo kuhusu vipengele mbalimbali vya ukosefu wa nidhamu

1.    Ukosefu wa nidhamu katika muda
Huyu kwa kweli ndiye adui mkubwa ambaye anazuia mafanikio makubwa ya watu wengi, kwani ana uwezo wa kupoteza, kuharibu na hata kufanya mipango ya mtu isitimie, kama tulivyomtazama kwa undani wake katika sura zilizotangulia.

Kusipokuwa na umakini katika kutumia muda, yaani kuwa mahali sahihi, ukifanya kitu sahihi kwa wakati sahihi lazima kunakuwa na upungufu katika kupata matokeo yaliyokusudiwa. Kama maandiko matakatifu yanavyo sema katika kitabu cha Mhubiri 3:1Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.”

Kwa hiyo tangu mbingu na nchi ziumbwe, mwanadamu aliumbwa ili afanye mambo yake yote kwa kufuata utaratibu. Mtume Paulo aliwaonya waefeso kuhusu kuutunza muda , alisema  “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; Mkiukomboa wakati kwa maana nyakati hizi ni za uovu” Waefeso 5:15-16

Na pia kuna usemi wa kiingereza usemao “you can choose to be the manager of time or the servant of time” it is your choice, ikimaanisha ya kwamba ni wewe tu mwenye maamuzi ya kutumia muda kwa kuuongoza (ukawa meneja) au ukaongozwa na muda (ukawa mtumwa). Hivyo ni vema kupata moyo wa hekima katika kuyafanyia kazi mafundisho haya nawe utakuwa mwenye hekima. Weka nidhamu ya hali ya juu katika kutumia muda wako.
2.    Ukosefu wa nidhamu katika mambo ya Mungu
Mungu wetu ni Mungu ambaye yuko makini na anayefuata utaratibu katika kufanya mambo yake yote. Katika siku sita za uumbaji aliumba kwa mpangilio thabiti na ndio matokeo mpaka sasa vitu vilivyoumbwa vipo. Vivyo hivyo kama wana wa Mungu aliye hai imetupasa kutii na kufuata maagizo anayotuagiza kila siku ili tuwe kama alivyotukusudia.
Wakristo wengi wamekuwa ni watu ambao wanapenda matokeo mazuri tu katika uhusiano wao na Mungu na kufikiri kwamba unakuja kiurahisi rahisi. Lahasha! Kuna juhudi zinatakiwa ikiwa na kufuata uongozi kwa ufasaha ndipo matokeo yanakuja.   katika kila jambo linahitaji kufuata uongozi wa neno la Mungu ambayo ndiyo nidhamu. Ni kweli yote yanawezekana kwa Mungu tukiamini na zaidi tukiwa na nidhamu kwa mambo yake.
3.    Ukosefu wa nidhamu katika kula/kunywa.
Unaweza dharau na kuona ni jambo dogo sana kutazama masuala ya afya ila hili ni jambo kubwa sana kwa kuwa mafanikio yako yanategemea sana afya yako ilivyo, kama afya yako si njema si rahisi kufikia malengo uliyonayo.
Tatizo si chakula ila tatizo ni wewe umekosa nidhamu katika matumizi ya chakula, kama una nidhamu nzuri utajua ni nini ukile kwa wakati fulani na nini usile kwa wakati fulani, ukifahamu kuwa kitu fulani kinaweza kuleta hatari ya afya yako nidhamu inakufundisha uache ili kuitunza afya yako iwe njema kukusaidia kutimiza malengo uliyonayo katika maisha yako. Mfano kuna watu wanavuta sigara na kunywa pombe wakifahamu kuwa ni hatari kwa afya zao na jamii iwazungukayo, jawabu rahisi kutoka kwao ni wamekosa nidhamu ambayo ingewasaidia kukwepa kwa kuwa nidhamu yatufunza kuwa makini kufanya mambo ya faida kwetu wenyewe.
Nidhamu katika mfumo mzima wa afya ni wa muhimu sana katika kuyafikia malengo au ndoto zako. Mungu wetu mwenyewe anataka tuwe na afya njema wakati wote ndio maana kwa kupigwa kwake msalabani sisi tumepona yaani tu wazima.
Ili tuweze kuwa na afya njema inatakiwa tujali afya za miili yetu kwa kutumia chakula bora pamoja na maji safi na salama.
Hapa nitatilia mkazo sana katika suala la kunywa maji, kwani mwili wetu umejengwa kwa asilimia 100 ambapo 60% ni maji na 40% ni chakula, kumaanisha ya kwamba 3/5 ya mwili ni maji tu na 2/5 ni chakula. Kwa hiyo inatakiwa tunywe maji kwa wingi na kwa kufuata utaratibu ili tuikinge miili yetu dhidi ya magonjwa, cha kushangaza watu wengi wanatumia chakula kwa wingi na maji yanatumiwa kama ya ziada tu, na zaidi utafiti unaonyesha ya kwamba 90% ya magonjwa yote huanzia kwenye mfumo wa mmeng’enyo wa chakula hivyo ni wazi kwamba kutozingatia kanuni sahihi za utumiaji wa lishe bora unapelekea kuibuka kwa magonjwa mengi.
Kwa kawaida kila mtu anapaswa kunywa maji yasiyopungua lita 3 kwa siku, lakini swali ni hili; je? Unakunywa kiwango sahihi, wakati sahihi, mahali sahihi ili uweze kupata matokeo sahihi? au matokeo yoyote? Unaweza ukasema huyu mwandishi anaongea nini, jibu ni kwamba kama unataka upate matokeo sahihi ni lazima ufuate kanuni sahihi. Hapa nitakufundisha kanuni rahisi sana itakayokusaidia kunywa maji na kupata matokeo mazuri maana imefanyiwa utafiti, kujaribiwa na hata kutumiwa kwa miaka mingi na matokeo tunayaona.
Kwanza unapoamka alfajiri kwa ajili ya maombi, mazoezi au kujiandaa ni lazima unywe 150cl ambayo ni sawa na lita 1.5 kwa muda wa dakika 2  ̶ 5. Na muda unaofaa ni (saa 10, 11 na 12) alfajiri kulingana na muda unaoamka ukichelewa sana saa 1 asubuhi. Imethibitishwa kwamba maji yanayonywewa muda huu yana umuhimu mkubwa sana katika ufanisi wa kazi zako za siku nzima.
Pili mchana saa moja kabla, au baada ya chakula kati ya saa7, 8 hadi 9 unakunywa 75cl ambazo ni sawa na 3/4 ya lita. Vivyo hivyo na jioni kati saa (12,1 na  2 )usiku unakunywa robo tatu ya lita yaani 1/2 +1/4.  Maji yanayoshauriwa kutumiwa ni ya kawaida usipende kutumia maji ya baridi. 

Ukianza kuifuata kanuni hii itakusaidia kufanya kazi kwa ufanisi, kwa muda mrefu na kuufanya ubongo wako ufanye kazi vizuri, pia itakukinga dhidi ya maradhi kwani kila sehemu ya mwili imepata kiasi chake cha maji kinachotakiwa. Sio hivyo tu bali utalala kwa wakati unaostahili kulala na utaamka kwa muda unaopaswa hivyo kuzuia kusinzia wakati wa kazi/ibaada/mikutano n.k.  Kwa wiki mbili za kwanza unapoanza unaweza ukaona ni kazi sana kwani unakunywa maji kwa muda usio na kiu bali kuanzia wiki ya tatu itakuwa ni tabia yako iliyojengeka na kuimarika na utayafurahia matokeo yake.
Pia kuhusu umuhimu wa maji katika Maisha ya mtu, naomba utafakari sana kuhusu UUMBAJI katika kitabu cha Mwanzo 1:2 “Nayo nchi ilikuwa ukiwa,tena utupu,na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji” Hivi? Kwanini roho wa Mungu alikaa juu ya maji na sio chini kwenye vilindi au mbinguni? Hii ni kuonyesha kwamba alikuwa anaatamia uumbaji (kuumbwa kwa nchi) hivyo hata kama hali uliyonayo ni ya ukiwa kiasi gani, maji ni ya muhimu sana katika kuumba afya njema.
Kwa kuwa afya njema ni ya muhimu sana kwa mafanikio ya mtu, Big Results Now (BRN) yaani matokeo makubwa sasa kwa afya yako yanawezekana kwa kufuata utaratibu sahihi ulioelekezwa. Wewe andaa maji yako tu, na uyatumie.
Daudi anamuomba Mungu na kumwambia “Basi utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima” na katika tafsiri ya The Living Bible usema “Teach us to number our days. And recognize how few they are, help us to spend them as we should,” utafsiri maneno haya kwa Kiswahili chake kuwa Utufundishe kuhesabu siku zetu. Tujue ni jinsi zilivyo chache, utusaidie kuzitumia jinsi itupasavyo.” Zaburi 90.12. Daudi kwa kuwa na hekima alifahamu kuna umuhimu sana wa kujua siku zake kuwa zi chache na kuna umuhimu mkubwa sana wa kuishi kwa hekima katika siku hizo. Ni dhahiri kuwa kama hujui kuwa una siku chache za kuishi duniani ni kazi kwako kuishi kwa hekima na hata kujua ni namna gani unapaswa kufanya hili afya yako iwe chache sana.
- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2015/05/somo-kukosa-nidhamu-ya-maisha-ni.html#sthash.pw7O4UEe.dpuf

No comments:

Post a Comment